• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

WAGANGA wa tiba za asili na mbadala wapewa Mafunzo Madaba

Posted on: September 26th, 2023

WAGANGA wa Tiba za asili Halmashauri ya  Wilaya ya Madaba wamepewa mafunzo ya kuzingatia miiko na maadili ya utoaji huduma kwa wagonjwa.

Mafunzo hayo yametolewa na Mratibu wa tiba asili na mbadala Shani Kabuga ,Afisa Lishe John Mapunda pamoja na   Mratibu wa Kifua Kikuu  na Ukoma Methew Mihangwa katika ukumbi wa Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Madaba.

Mihangwa ameeleza kuwa Mganga wa tiba za asili endapo atapata dalili za ugonjwa wa TB anapaswa kuwahishwa kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya mara moja.

Mratibu wa Kifua kikuu na Ukoma ameeleza dalili hizo ikiwa ni pamoja na Mgonjwa kutokwa na Jasho jingi usiku, kukohoa sana zaidi ya siku saba,homa za mara kwa mara,vikohozi vilivyochanganyika na damu pamoja na maumivu ya mifupa.

Kwa upande wake Mratibu wa tiza za asili na tiba mbadala Shani Abdul Kabuga amesema  kanuni taratibu na sheria za waganga  wa asili na mbadala,kanuni zinazosimamia utekelezaji wa sheria na 23 ya 2002,adhabu za kisheria  kwa mganga au msaidizi wa tiba za asili anayetoa huduma kinyume na sheri pamoja na mambo yote yaliyokatazwa katika tiba za asili.

Afisa Lishe Halmashauri ya Madaba John Mapunda katika mafunzo hayo ya waganga wa tiba asili na mbadala amehimiza kuhakikisha wanawatambua wateja wenye utapiamlo na kuwashauri kwenda kwenye vituo vya huduma ya Afya badala ya kuendelea kuwaweka katika maeneo yao ya matibabu jambo ambalo linaweza kuhatarisha maisha mfano kwashakoo,unyafuzi,pamoja na upungufu wa Damu.

Imeanadaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

Septemba 26,2023.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa