• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

UFUTA wawaingizia wakulima Ruvuma bilioni 25

Posted on: February 11th, 2021

WAKULIMA mkoani Ruvuma wamefanikiwa kuingiza zaidi ya shilingi bilioni 25 baada ya kuuza kilo 12,234,757 ya zao hilo kupitia mfumo wa stakabadhi ya mazao ghalani kuanzia msimu wa mwaka 2018/2019 hadi 2019/2020.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amesema katika kipindi hicho wakulima pia walifanikiwa kuuza kilo 1,499,077 zilizowaingizia zaidi ya shilingi bilioni moja na zao la mbaazi ambalo liliwaingizia zaidi ya shilingi bilioni 2.585 baada ya kuuza kilo 4,260,777.

“Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa mikoa ambayo imekuwa inatekeleza mfumo wa stakabadhi ya mazao ghalani,pia tuna mazao mawili ya kimkakati ambayo ni korosho na kahawa,yamekuwa yakiuzwa kupitia mfumo huu’’,alisema Mndeme.

Amesema mfumo huo umewanufaisha wakulima kwa kupata soko la uhakika na bei nzuri ya mazao yao na kwamba shughuli za kilimo katika msimu wa mwaka 2020/2021 zinaendelea vizuri ambapo wakulima wamelima mazao mbalimbali.

Kuhusu mbolea,Mkuu wa Mkoa amesema Mkoa kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mbolea Tanzania(TFRA) unaendelea kusimamia upatikanaji wa mbolea ili wananchi waweze kuzalisha chakula cha kutosha.

Hata hivyo amesema hadi kufikia Novemba 2020 jumla ya tani 31,624 za mbolea zilikuwa zimeingia mkoani Ruvuma kati ya mahitaji ya mbolea tani 50,524.50.

Mkoa wa Ruvuma umekuwa gwiji katika uzalishaji wa mazao ya chakula nchini,baada ya kushika nafasi ya kwanza kitaifa miaka miwili mfululizo,msimu wa mwaka 2018/2019 na 2019/2020.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Mkoa wa Ruvuma

Februari 11,2021

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa