• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

TASAF yawaneemesha wanufaika Halmashauri ya Madaba

Posted on: November 29th, 2022

AGNES Mgimba ni mkazi wa Kijiji cha Kipingo Kata ya Lituta ni mnufaika wa mpango wa TASAF kwa mda wa zaidi ya miaka mitano.

Afisa maendeleo ya Jamii Juma Komba Halmashauri ya Madaba ametembelea Kaya hizo na kuangalia jinsi mnufaika huyo alivyojiwekeza katika ufugaji na kuepukana na umaskini.

Mgimba amesema TASAF imemsaidia kwa kusomesha watoto ikiwemo mmoja kufika chuo kikuu na wawili kumaliza kidato cha nne, pamoja na kuwa na chakula cha kutosha na familia kuwa na furaha ya maisha.

“Mpango wa TASAF kabla haujaanza nilikuwa na hali duni sana,nimesomesha wanangu,nilikuwa sina chakula kwa sasa ninachakula cha kutosha,nina maji pamoja na umeme na ufugaji wa kuku na hii ni awamu ya pili sasa na fuga na nilipata faida ya laki tano”.

Hata hivyo mama Mgimba  amempongeza Rais wajamhuri ya muungano wa Tanzania Rais Samia kwa kuhakikisha TASAF inawasaidia watu Maskini na kuondokana na hali ngumu ya Maisha.

“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mimi nashururu sana kwa kuangalia watu wa hali ya chini nilikuwa nalazwa mara kwa mara nilikuwa na mawazo mengi ,nilitelekezwa na mumewangu zaidi ya miaka 10 watoto wakiwa wadogo”.

Kwa upande wake Mnufaika wa TASAF Selina Kisite kutoka Kijiji cha Ifugwa ameelezea namna ambavyo Mpango wa TASAF ulivyomnufaisha mara baada ya kuachwa na Mume wake zaidi ya miaka 15.

Amesema Mpango wa TASAF Ulimsaidia kusomesha watoto pamoja na ufungaji wa Mbuzi zaidi ya 10,Kuku zaidi ya 20 pamoja na ujenzi wa nyumba ya kuishi na kuepukana na Nymba za kupanga.

Kisite ameeleza namna ambavyo kupitia hela hizo za TASAF licha ya kufuga mifugo mbalimbali alikuwa analima bustani ya mbogamboga nakumsaidia kupata kipato zaidi na kupelekea maisha yake kuwa mazuri.

“Mimi nilikwa nikipokea hela kutoka TASAF nilikuwa nagawa katika kilimo cha bustani,Ufugaji wa Kuku na Mbuzi ikanipelekea kujenga nyumba yangu na kuepuka  na Nyumba za kupanga miaka mingi baada ya kuachana na mume wangu”.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Habari  Halmashauri ya Madaba

Novemba 29,2022.

 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa