• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

TARURA Madaba walivyojenga Daraja la Mawe kwa teknolojia rahisi

Posted on: March 21st, 2023

WAKALA wa barabara za vijijini na mijini(Tarura)imekamilisha ujenzi wa daraja lililojengwa kwa teknolojia ya mawe katika mto Mgombezi  linalounganisha kijiji cha Lipupuma,Mgombezi na Chechengu katika Halmashauri ya Madaba wilayani Songea.

Meneja wa TARURA Wilaya ya Songea Bakari John alisema,daraja la mto Mgombezi lina urefu wa kilomita 41 na ujenzi kwa kutumia teknolojia ya mawe ni wa gharama nafuu na la kwanza kujengwa wilayani Songea.

Alitaja gharama za ujenzi wa daraja hilo ni shilingi milioni 152 tu na kueleza kuwa, kama wangejenga kwa kutumia zege  na chuma kama ilivyo kwa madaraja mengine basi serikali ingetumia zaidi ya shilingi milioni 500.

Alisema,kabla ya ujenzi wa daraja hilo wananchi walilazimika kupita kwenye daraja la miti lililojengwa na wananchi wenyewe,hata hivyo wakati wa masika halikuwasaidia kutokana na mto Mgombezi kujaa maji mengi na kukatisha mawasiliano kati ya upande mmoja na mwingine.

Alieleza kuwa, kujengwa kwa  daraja hilo ni ukombozi mkubwa kwa wananchi wa maeneo hayo kwani limetatua kero ya muda mrefu ya usafiri na usafirishaji wa mazao hasa mbao na Tangawizi.

Meneja huyo wa Tarura aliongeza kuwa, kazi iliyobaki ni kuendelea kufungua barabara za kuunganisha mashamba  ili kuwawezesha wananchi  kuendelea na shughuli zao za kilimo kwa urahisi.

Baadhi ya wananchi waliokutwa wakivuka katika daraja hilo,wameishukuru serikali  kwa uamuzi wake wa kujenga daraja la kudumu kwani kwa muda mrefu walikuwa wakiteseka kupita kwenye maji pindi wanapohitaji kuvuka upande mmoja kwenda mwingine.

Nuru Francis  mkazi wa Lipupuma alisema,walikuwa na hali mbaya  kwani walilazimika kupita kwenye mto huo wenye maji mengi  kila siku na wakati wa masika walishindwa kwenda kwenye shughuli zao za uzalishaji mali kutokana na mto huo kujaa maji.

Michael Brumo,ameipongeza serikali ya awamu ya sita  kuona umuhimu wa kujenga daraja katika eneo hilo kwa sababu ilikuwa changamoto kubwa kila wanapotakakusafirisha mazao yao kutoka shambani kwenda sokoni.

Robert Mbilinyi,ameishauri serikali kuendelea kujenga madaraja kwa kutumia teknolojia ya mawe ambayo ni ya gharama nafuu na kuachana na ujenzi wa madaraja ya chuma ambayo wakati mwingine baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu wanahujumu kwa kuiba vyuma na hivyo kuisababishia serikai hasara kubwa.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa