• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

SERIKALI yatoa milioni 50 ujenzi wa nyumba ya Mwalimu Matazamo Madaba

Posted on: February 17th, 2023

WATAALAMU kutoka ofis ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma wametembelea na kukagua Miradi  katika Halmashauri ya Madaba.

Moja kati ya Mradi huo waliotembelea ni Nyumba ya Mwalimu Shule ya Msingi Mtazamo Kata ya Mkongotema Kijiji cha Lutukila inajengwa kwa milioni 50.

Akisoma taarifa hiyo Makamu mkuu wa Shule hiyo Slavian Kingilo amesema mradihuo unatekelezwa kupitia fedha kutoka Serikali kuu na mradi huo umeanza kutekelezwa rasmi Novemba 29,2022.

Kingilo amesema mradi huo unatekelezwa kupitia utaratibu wa force account ambapo shule inanunua vifaa na kuajiri fundi ujenzi kwa mkataba wa muda mfupi wa ujenzi.

Hata hivyo amesema hatua ya ujenzi wa mradi huo umefikia katika hatua ya kupandisha kuta za juu ya lenta ikiwa jumla ya fedha zilizotumika mpaka kufikia sasa ni zaidi ya shilingi milioni 25.

“Faida za mradi huo nipamoja na kupunguza adha ya makazi kwa walimu,kuongeza tija na ufanisi wa kuinua taaluma mashuleni”.

Makamu Mkuu wa Shule hiyo amezitaja changamoto mbalimbali zilizojitokeza ikiwemo  ukosefu wa maji katika eneo la ujenzi ambapo imeongeza gharama za ujenzi kwa kununua maji kwa gharama kubwa pipa moja shilingi 5,000/=, kupanda kwa ghara za vifaa vya ujenzi kama vile nondo,bati na Saruji.

Kingilo amesema utatuzi wa changamoto hizo ni pamoja na kutafuta wazabuni wenye gharama nafuu za vifaa ili kupunguza ongezeko kubwa la fedha iliyo nje ya BOQ.

Hata hivyo Makamu Mkuu wa Shule ametoa shukrani kwa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia fedha kwaajili ya ujenzi wa nyumba ya Mwalimu ambayo ikikamilika itasaidia kutatua adha ya makazi kwa walimu.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Feburuari 17,2023.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa