• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

SERIKALI ya awamu ya Sita ilivyotatua changamoto ya Miundombinu ya Sekondari Wino

Posted on: October 5th, 2023

UONGOZI wa Shule ya Sekondari Wino Halmashauri ya Madaba wameipongeza Serikali kwa kuwapelekea fedha zaidi ya shilingi Milioni 402 kwaajili ya ujenzi wa miundombinu ya Shule Mwaka wa fedha 2020/2023.

Akisoma taarifa Mkuu wa Shule hiyo Kelvin Mwinuka katika sherehe za Mahafari ya 15 ya kidato cha nne yaliyofanyika leo Shuleni hapo wanafunzi 113 wanatarajia kuhitimu mwezi Novemba 2023.

 Mwinuka amemshukuru Mbunge wa Jimbo la Madaba Joseph Mhagama kwa kuwanunulia wanafunzi Runinga ya Shule ambayo inawasaidia kuangalia habari mbalimbali zinazoendelea katika nchi ya Tanzania.

“Wino Sekondari tumepokea kiasi cha shilingi 402,072,379.85 kwaajili ya ujenzi wa miundombinu ya Madarasa,bweni la wavulana,nyumba za Walimu na Miundombinu ya Maji pamoja na ukamilishaji wa bwalo la chakula”.

Hata hivyo Mkuu wa Shule hiyo ameendelea kuwapongeza wadau mbalimbali akiwemo Wakala wa Misitu Wino (TFS) kwa kutatua changamoto mbalimbali kama vile ujenzi wa chanzo cha Maji,viti na Meza kwaajili ya  Walimu,upandaji miti na utunzaji wa Mazingira.

Kwaupande wake Meneja wa Shamba la Miti Wino Grory Fotnatus akiwakilishwa na Afisa Misitu Geofrey Shio amesema kupitia changamoto zilizopo shuleni hapo watakarabati jengo la utawala wakisaidiana na wazazi kupitia zoezi la keki  ambapo zimepatikana kiasi cha  zaidi ya shilingi  laki nane katika mahafari hayo.

Mwenyekiti wa Halmashauri  ya Madaba Teofanes Mlelwa amemwakilisha Mgeni rasmi katika Mahafari hayo Mbunge wa Jimbo la Madaba Joseph Mhagama akiwa Amerca Kusini akiliwakilisha Bunge la Tanzania  na  Spika wa Bunge Tulia Akson.

Mlelwa amewapongeza wanafunzi hao kwa kutimiza miaka mine wakiwa shuleni hapo na kuwasisitiza kusoma mda uliobaki ili waweze kufaulu masomo yao ikiwa mwaka 2022 Matokeo ya kidato cha nne katika shule hiyo walipata asilimia 100.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Octoba 5,2023.

 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa