• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

RUVUMA yaongoza tena utoaji wa chanjo ya polio

Posted on: June 2nd, 2022

Jumla ya watoto 12,131,049 sawa na asilimia 117.8 wamepatiwa chanjo ya matone dhidi  ya ugonjwa wa Polio kwa watoto chini ya miaka mitano kati ya watoto 10,295,316 waliolengwa kwenye kampeni ya Chanjo iliyofanyika nchini tarehe 18 hadi 21 Mei mwaka huu.

Hayo yamebainishwa leo na Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu wakati akitoa tathimini ya kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya Ugonjwa wa Polio kwa watoto chini ya miaka mitano nchini kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

Waziri Ummy amesema idadi hiyo iliyofikiwa ni mafanikio makubwa kama nchi na kutoa pongezi kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya,Timu za uendeshaji wa huduma za afya ngazi ya Mikoa na Halmashauri ,watumishi wa afya pamoja na wadau mbalimbali wakiwemo wadau wa maendeleo kwa kusimamia kikamilifu maandalizi ,uzinduzi na utekelezaji wa kampeni katika maeneo yao kwa umahiri mkubwa.

"Nawapongeza pia wazazi na walezi wote kwa kuitikia wito wa Serikali kwani afua ya chanjo ni muhimu kwa watoto katika kuwalinda dhidi ya magonjwa yanayo zuilika kwa chanjo".

Waziri Ummy aliutaja Mkoa wa Ruvuma umeongoza kwa kuvuka lengo kwa 131%, ikifuatia na Shinyanga 128%, Rukwa 123%, Pwani 122%, Arusha 122%, Mbeya, Geita, Dar es Salaam na Simiyu yote ina 121%, Singida, Dodoma na Tabora 118% , Kigoma, Njombe, Katavi 117%, Morogoro 116%, Mara, Mtwara, Lindi na Tanga  115%, Kilimanjaro na Mwanza 114%, Manyara na Iringa 113%, Songwe na Kagera 111%.

Hata hivyo Waziri Ummy ametoa wito kwa Viongozi,wadau na wazazi kutoa ushirikiano kwa kampeni zinazofuata ambazo zinatarajiwa kufanyika mwezi Julai na Agosti mwaka huu.

Ameongeza kuwa tunayo kila sababu ya kuilinda nchi yetu na watoto wetu dhidi ya ugonjwa wa Polio.'Mzazi/Mlezi hakikisha watoto wanapata chanjo ya Polio,bado tunaweza kutunza rekodi ya Tanzania kuwa nchi isiyokuwa na ugonjwa wa Polio duniani.

Kampeni ya Polio inatakiwa kufanyika kila baada ya wiki nne ili kuhakikisha watoto wote wanafikiwa kulingana na mwongozo wa WHO wa kukabiliana na ugonjwa wa Polio unaelekeza kuwa endapo mlipuko wa ugonjwa umetoke nchi  ambayo mlipuko umetokea pamoja na zile zinazozunguka zinapaswa kufanya kampeni za kutoa chanjo ya polio mara nne mfululizo pamoja na kutoa chanjo kwa watoto wote walio chini ya miaka mitano ili kuzuia kusambaa kwa maambukizi ya ugonjwa huu.

Imeandikwa na Catherine Sungura w Wizara ya Afya 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa