• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

RUVUMA yafanya jitihada za kuongeza thamani ya Maziwa

Posted on: September 15th, 2022

Mkoa wa Ruvuma umefanya jitihada za kuimarisha na kuongeza thamani  ya Maziwa katika Halimashauri zake.

Afisa Mifugo Mkoa wa Ruvuma Nelson  William amesema wamefanya uchunguzi wa Magonjwa kifua kikuu (TB) na ugonjwa wa kutupa mimba (brucellosis) kwa Ng’ombe wa maziwa 1,546.

Amesema katika Halmashauri za Wilaya ya Namtumbo,Songea na Manispaa  ya Songea Mkoa umehamasisha wasindikaji wadogo wadogo wa Maziwa kwa sasa kuna jumla ya wasindikaji 6 wanasindika kwa wastani wa lita 201,600 kwa mwaka.

Hata hivyo Afisa Mifugo amesema mfumo wa utambuzi  na ufuatiliaji wa Mifugo Tanzania unasimamiwa kwa Sheria ya Usajili Na 12 ya Mwaka 2010 na kanuni zake za mwaka 2011.

“Kwa Mkoa wetu wa Ruvuma Halmashauri ziko kwenye hatua tofauti ya maandalizi ya kutekeleza zoezi hili”.

Amesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Mkoa wametoa Elimu kwa Wakuu wa Wilaya,Wakurugenzi wa Halmashauri,Wakuu wa Idara za Mifugo na Uvuvi Maafisa Tehama pamoja na Maafisa Utambuzi wa Halmashauri.

Afisa mifugo amesema zoezi la utambuzi litasaidia kudhibiti wizi wa mifugo pamoja na kuthibitisha umiliki wa mifugo hiyo ikiwemo fursa ya kibiashara ya Kimataifa kwa kukidhi viwango vya ushindani na soko la kimataifa.

William amezitaja changamoto katika Sekta ya Mifugo ikiwemo Ukame maeneo ya ranchi ndogo na ukosefu wa miundombinu ya maji  Majosho  pamoja na ukosefu wa kudhibiti Magonjwa kliniki za mifugo.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Septemba 16,2022.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa