• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

RUVUMA yadhamilia kupunguza udumavu

Posted on: February 16th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amesema udumavu bado changamoto  ambapo takwimu zinaonesha Mkoa una udumavu kwa asilimia 35.6.

Kanali Thomas amesema hayo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa  utekelezaji wa mkataba wa lishe  uliofanyika katika ukumbi wa Chandamali Manispaa ya Songea.

Amewaagiza waganga wakuu wa Wilaya kuendelea  kusimamia utekelezaji wa masuala ya lishe katika afua mbalimbali kuanzia ngazi ya jamii,vituo vya tiba,ngazi ya kata ,vijiji na mitaa.

“Bado hatufanyi vizuri katika eneo la udumavu,Mkoa wetu udumavu ni asilimia 35.6,hivyo lazima mtambue kuwa bado tuna kazi kubwa ya kusimamia afua za lishe katika ngazi ya jamii na vituo vya kutolea huduma za afya’’,alisisitiza.

Amesema kufanyika kwa mkutano huo ni muendelezo wa utekelezaji wa maelekezo yaliyotolewa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan jijini Dodoma Septemba 30,2022.

 Amesisitiza  kuwa Mkoa wa Ruvuma utaendelea kufanya tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa lishe mara mbili kwa mwaka na kwamba Halmashauri zote zitafanya tathimini hiyo kila robo ya mwaka ambapo amewaagiza wakuregenzi watendaji kushirikiana na waganga wakuu kusimamia utekelezaji wa masula ya lishe.

Amewaagiza wakuu wa shule kuhakikisha kila shule inatoa huduma ya chakula kwa uhakika kwa wanafunzi wote badala ya kutoa chakula kwa madarasa ya mitihani yakiwemo darasa la nne,kidato cha pili na cha nne huku madarasa mengine yakipata chakula kwa idadi ndogo.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa ameagiza kutafutia majawabu ya tatizo la ukosefu wa virutubishi katika vyakula vinavyoliwa shuleni.

Mkuu wa shule sekondari ya Wavulana Songea Mwl.Gerasias Lugome akizungumza kwenye kikao  hicho cha tathmini ya lishe,ametoa rai kwa wakuu wa shule na wadau wa elimu kuzingatia utoaji lishe kwa wanafunzi ili kupunguza udumavu ambao ambao unachangia kushusha taaluma shuleni.

Mikoa yenye  mitano yenye  kiwango kikubwa cha udumavu nchini ni Pamoja  na Iringa inayoongoza kwa asilimia 56.6,Njombe asilimia 50.4,Rukwa asilimia 49.8,Geita asilimia  38.6 na Ruvuma asilimia 35.6

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa