• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

RC Ruvuma atembelea Madaba kuona wanafunzi walioripoti Shuleni

Posted on: January 8th, 2024

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas leo Januari 8,2024 ametembelea shule mpya ya  Msingi Lipupuma iliyojengwa kwa shilingi Milioni 331 na Sekondari ya Lilondo iliyojengwa kwa shilingi Milioni 560 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.

Lengo la Ziara hiyo kuona wanafunzi wa Kidato cha kwanza waliopangiwa kujiunga mwaka huu 2024 katika Shule ya Sekondari Lilondo  na shule ya Msingi Lipupuma ambayo wamegawa wanafunzi kutoka shule ya Mkongotema.

“Tumeona wanafunzi wameanza kukaa madarasani katika shule ya Msingi Lipupuma,maelekezo yalikuwa leo watoto waanze kuingia darasani kabla ya wiki hii kuisha watoto wote wanaotakiwa kujiunga na shule ya Lilondo wawe wemeripoti”.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa amesema kwa kuwa Shule ya Lilondo imejengwa madarasa yanayojitosheleza wagawe wanafunzi kutoka shule ya Sekondari Wino madarasayatimie  hadi kidato cha nne.

“Hapa wamepangiwa wanafunzi 118 ambao wataingia katika madarasa haya na madarasa mengine hakikisheni wanafunzi mnawagawa kutoka shule mama ya Wino Sekondari”.

Hata hivyo Thomas amewapongeza wananchi wa Lilondo kwa kujitoa kwa nguvu zao katika kuanzisha shule hiyo  na kujenga madarasa ambayo yatatumika kama hosteli kwa wanafunzi pamoja na nyumba za walimu.

“Kilichonifurahisha Rais wa awamu ya sita baada ya kusikia kilio chenu akaamua kuleta mzigo  wa Milioni 560 wa kujenga shule nzima na ninyi madarasa yenu mliyojenga kwa nguvu zenu mmeamua kufanya hosteli kwaajili ya watoto watakaosoma katika shule hii hongereni sana”

Mkuu wa Mkoa ametoa rai kwa uongozi wa Halmshauri hiyo kuhakikisha wanaweka miundombinu itakayowasaidia wanafunzi kuishi katika hosteli ikiwemo vyoo,bafu na sehemu ya kufulia.

Kutoka kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Januari 8,2024.

 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa