• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

RC Ruvuma amwagiza Dc Songea kukamata wazazi ambao hawatapeleka watoto Shule

Posted on: July 1st, 2023

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Kanal Laban Thomas amemwagiza mkuu wa Wilaya ya Songea Wilman Ndile kuwakamata wazazi ambao hawatapeleka watoto shule.

Hayo amezungumza alipotembele Halmashauri ya Wilaya ya Madaba na kukagua Miradi ya Boost inayojengwa katika Shule sita za Msingi na awali inayogharimu kiasi cha shilingi Milioni 610,300,000/= na miradi ya Swash inayojenga matundu ya vyoo na uwekaji wa miundombinu ya maji taka katika Shule za Msingi 11 kiasi cha shilingi Milioni 436,359,306.

Mkuu wa Mkoa amesema wazazi wahakikishe watoto wanaenda shule akisoma hata kama hatapata ajira akiingia katika Kilimo atalima kwa kitaalam zaidi tofauti na ambae hakwenda Shule.

“Mh. Mkuu wa Wilaya nakuaminia sana watoto ambao hawaendi Shule kamata wazazi Serikali inaleta hela kujenga shule Watoto waende shule Elimu Pekeake ndio itatukomboa”.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa amesisitiza wananchi kulima kwa kilimo cha kisasa kuhakikisha heka moja kuweka mifuko 3 ya Mbolea itakayopelekea kuvuna mavuno mengi.

Hivyo amesema kwa wakulima kupitia kipindi hiki cha Mavuno kuhakikisha wanaweka chakula na kuimarisha vyama vya ushirika na kuhakikisha wanauza mazao kwa mfumo wa stakabadhigharani.

Amesema katika Halmashauri ya Madaba ardhi yake yanastawi  Mazao  mengi  yakiwemo mazao ya Ufuta,Mbaazi,Soya,Alizeti,Mahindi,Maharage,Tumbaku,pamoja na Tangawizi

Mkuu wa Mkoa ametoa rai kwa wananchi kuuza Mahindi NFRA kwa bei ya shilingi 700 kwa kilo na kuacha kuuza kwa walanguzi mtaani ambao wanatumia dumla na kuwaibia wananchi.

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Julai 1,2023.

 

 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa