• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

RC IBUGE:Wataalamu wa afya Ruvuma toeni elimu endelevu kwa wananchi kujikinga na corona

Posted on: July 14th, 2021

RC IBUGE;WATAALAMU WA AFYA TOENI ELIMU ENDELEVU YA KUJIKINGA NA CORONA KWA WANANCHI

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge ameziagiza Halmashauri zote nane kupitia wataalam wa afya kusimamia kutoa elimu ya kujikinga na  maambukizi ya wimbi la tatu la corona.

RC Ibuge ametoa maagizo hayo wakati anazungumza na  wakuu wa wilaya,wakurugenzi wa Halmashauri na watumishi wa umma ngazi ya Mkoa na wilaya zote kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Amesisitiza elimu endelevu ya kujikinga kabla ya kuugua  corona itolewe kwa wananchi ikiwemo kuvaa barakoa,matumizi ya kunawa kwa sabuni na maji titirika na kuepuka mikusanyiko isiyokuwa ya lazima.

“Nimepita na kuzunguka baadhi ya maeneo mjini Songea,nimeona wananchi wameacha zile hatua ambazo tulikuwa tumezichukua katika wimbi la kwanza mfano,nje ya maeneo ya huduma,ndoo hazina maji wala sabuni,tukasimamie kuwaelimisha wananchi kwa sababu kujikinga ni gharama ndogo kuliko kutibu’’,alisisitiza RC Ibuge.

Amesisitiza kuwa corona ipo nchini,ingawa amebainisha kuwa katika Mkoa wa Ruvuma tishio la corona sio kubwa,hata hivyo amesema hakuna mipaka iliyofungwa  hivyo kuna mwingiliano mkubwa wa watu kusafiri na kuingia ndani ya Mkoa wa Ruvuma hivyo elimu endelevu ya kujikinga na corona isimamiwe ipasavyo kwa wananchi.

“Suala la  kujikinga ni rahisi kuonekana halina umuhimu kama madhara bado hatujayaona,sote tumekuwa tukisikia maelekezo mbalimbali kutoka Wizara ya Afya na kupitia viongozi wa kitaifa akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,wimbi la tatu la corona tayari lipo nchini tuchukue tahadhari’’,alisema RC Ibuge.

Takwimu kutoka Wizara ya Afya zinaonesha kuwa hadi sasa Tanzania ina wagonjwa wa corona 408 waliothibitika kutoka baadhi ya mikoa hapa nchini.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa