• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

RC IBUGE awaagiza watendaji wasisubiri migogoro ya ardhi iwakute ofisini

Posted on: July 13th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amewaagiza maafisa wa ardhi kutatua migogoro ya ardhi kwa kuwatembelea wananchi katika maeneo yao badala ya kusubiri migogoro hiyo kuwakuta maofisini.

RC Ibuge ametoa maagizo hayo  wakati anazungumza katika kikao kazi cha watumishi wa sekta ya ardhi mkoani Ruvuma ambacho kimeshirikisha watendaji mbalimbali wakiwemo wakuu wa Wilaya,wakurugenzi wa Halmashauri,makatibu Tawala wa wilaya na watumishi wengine ngazi ya wilaya na Mkoa kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Maelekezo mengine ambayo ameyatoa RC Ibuge kwa maafisa ardhi ni kuhakikisha wanafanyakazi kwa weledi na kwa kuzingatia maadili ya kazi,kutojiuhusisha kuomba na kupokea rushwa na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu sheria mbalimbali za ardhi.

“Ikumbukwe kuwa baadhi ya migogoro ya ardhi hutokea kutokana na wananchi kutofahamu sheria za ardhi,kwa hiyo kinachohitajika hapa ni uelewa wa sheria ili wananchi kuzifahamu’’,alisisitiza Ibuge.

Brigedia Jenerali Ibuge pia ameagiza kuendelea na ukamilishaji wa kazi zote za urasimishaji wa makazi holela katika Halmashauri zote za Mkoa wa Ruvuma na kwamba kipaumbele kiwa katika  Halmashauri ya Manispaa ya Songea ambapo zoezi hilo linafanyika kwa kasi ndogo ukilinganisha na wingi wa maeneo yaliyojengwa kiholela.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa  ametoa rai kwa wananchi ambao maeneo yao yamechukuliwa kwa ajili ya uwekezaji na yanahitaji fidia kuendelea kuwa watulivu wakati serikali inatafuta fedha kwa ajili ya fidia.Maeneo yanayohitaji fidia yaliyopo Manispaa ya Songea ni Bonde la Mto Ruhila,eneo la EPZA Kata ya Mwengemshindo na barabara ya  By Pass ya Mtwara Corridor.

Katika kikao kazi hicho RC Ibuge amewaagiza wanasheria wa Halmashauri zote kwa kushirikiana na maafisa Ardhi na TAKUKURU  kutoa elimu ya namna bora ya kufany usuluhisho wa migogoro ya ardhi kwa wajumbe wa Mabaraza ya Ardhi ya Kata kwa sababu wameonekana kuwa sehemu ya kikwazo katika kutenda haki kwa wananchi.

Akizungumza kwenye kikao hicho,Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema ameshauri ili kutatua changamoto za ardhi,bajeti ya kupima ardhi iongezwe ili eneo kubwa la ardhi lipimwe kuepusha migogoro ambayo inatokana na maeneo mengi kutopimwa.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Julai 13,2021

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa