• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MWENYEKITI Madaba atoa rai kwa wazazi,walezi kuzingatia malalezi bora ya watoto

Posted on: June 16th, 2023

HALMASHAURI ya Wilaya ya Madaba wameadhimisha siku ya Mtoto wa Afrika kwa kutoa huduma  mbalimbali  za kijamii kwa Wanafunzi wa Shule ya Msingi Matetereka.

Maadhimisho hayo yamefanyika katika Kijiji cha Matetereka  Kata ya Matetereka,Mwenyekiti wa Halmashauri  hiyo Teofanes Mlelwa amekuwa Mgeni Rasmi katika maadhimisho hayo.

Mlelwa amewataka wazazi na viongozi kutimiza wajibu wao katika kuhakikisha mtoto anapata mahitaji  na haki yake ya msingi.

Amesema kila tarehe 16 Mwezi Juni ni siku ya Kimataifa ya mtoto wa Kiafrika ambayo dunia inakumbuka watoto takribani 700 waliouawa  wakati wa maandamano yaliyozua ghasia mji wa Soweto  Afrika Kusini.

Hata hivyo amesema maandamano hayo yalizua taharuki na umwagaji wa damu yalijukana kama mauaji ya Soweto yaliyatumika kuhamasisha kwa jamii  kuboresha  mahitaji endelevu kama Elimu  kwa watoto barani Afrika.

“Siku hiyo tarehe 16 mwaka 1976 zaidi ya wanafunzi 2000 wa Afrika kusini waliandamana mtaani wakitaka kuboresha Elimu ikiwemo kufundishwa kwa Lugha yao wenyewe baada ya lugha ya Kingereza na kuondoa mfumo wa ubaguzi wa rangi kwani uliowatenga wanafunzi weusi na wazungu “

Amesema ilipofika mwaka 1991 kutokana na uzito wa tukio lililoacha majonzi kwa jamii ya kiafrika na umoja wa OAU iliweka adhimio ya kuitambua siku ya tarehe 16  kila mwaka kuwa siku ya mtoto wa Afrika na kutambuliwa Duniani kote .

“Siku hii ya tarehe 16 Juni inalenga kuondoa vizuizi vinavyowakabili watoto wa Tanzania na Afrika kupata haki zao katika Nyanja zote ikiwemo Elimu bora,Afya,Malezi, ulinzi pamoja na kutokomeza ukatili dhidi ya watoto”

Halmashauri ya Madaba wameadhimisha kwa kauli mbiu isemayo ondoa vikwazo mwezeshe mtoto kutimiza ndoto zake,wakiungana na Waafrika wote kwa kujenga mifumo bora ya malezi itakayompa mtoto  malezi bora huduma za Afya Elimu  na haki zote za Msingi kama ilivyo katika sheria za Nchi na Kimataifa.

Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Matetereka Restuta Mgaya akisoma Risara katika Maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika kwa Mgeni rasmi amesema kauli mbiu ya mwaka 2023 inayosema zingatia Usalama wa Mtoto katika ulimwengu wa kidijitali kupitia kauli mbiu hiyo walimu,wazazi na jamii wanatakiwa kufahamu madhara  ya matumizi yasiyo sahihi ya mitandao kwa watoto.

Amesema matumizi ya mtandao kwa mtoto yanapelekea kwenda kinyume na sheria ya mtoto badala yake walindwe na kuongozwa  kwenye matumizi ya vifaa vya kidijitali ikiwemo simu za mkononi,Runinga,Komputa na vishikwambi kwa sababu vifaa hivyo kupelekea maudhui yasiyofaa kwa watoto.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Juni 16,2023.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa