• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MWENGE wa Uhuru Aprili 19 utapokelewa Madaba kutoka Wilaya ya Namtumbo

Posted on: March 14th, 2023

HALMASHAURI ya Wilaya ya Madaba wamefanya kikao cha wadau wa Mwenge wa Uhuru unaotarajia kufika Mkoa wa Ruvuma Aprili 17.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo  Sajidu Idrisa Mohamed akizungumza katika kikao hicho amesema lengo la kuwaita wadau  ili  kuwaeleza  juu ya Mwenge wa Uhuru unaotarajia kufika katika Halmashauri hiyo Aprili 19 na kukagua pamoja na  kuzindua miradi mbalimbali ya Maendeleo.

“Aprili 19,2023 tutaupokea Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri yetu ya Madaba kutoka Wilaya ya Namtumbo  namapokezi yatafanyika katika Shule ya Msingi Likalangiro Kata ya Mtyangimbole”.

Mkurugenzi amesema kuanzia sasa Mbio za Mwenge wa  Uhuru katika Halmashauri hiyo umeanza kwa kuandaa miradi na uhamasishaji kwa wananchi ili wajue tukio muhimu linakuja.

“Sisi kama wadau na viongozi tukawaambie wananchi Mwenge wa Uhuru unakuja katika Halmashauri yetu ya Madaba,kwa maana hiyo kupitia Mwenge wa uhuru unamwakilisha  Rais wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hii ni heshima kubwa katika Halmashauri yetu”.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Teofanes Mlelwa katika kikao hicho cha wadau amesema amefurahishwa na ujio wa wadau  kwa kushiriki Kikao hicho ikiwa  linapotokea jambo la muhimu kama Mwenge wa Uhuru kuwe na ushirikishwaji  kwa wanadu mbalimbali na wananchi.

“Mwenge wa uhuru unapokuja katika Maeneo yetu unapita kwenye miradi ambayo ni yawananchi tuhakikishe tunakesha nao wote tumeona vema kuwakaribisha wadau kwa  kutii na kuja”.

Mlelwa ametoa rai kwa wananchi kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi siku hiyo ya kuupokea Mwenge wa Uhuru bila kupuuza ikiwa Mwenge unakuja kwaajili ya wananchi wote siyo viongozi wa Serikali pekee.

Kwa upande wake Mchungaji wa Kanisa la KKT Madaba Faraja Kisosho katika kikao hicho cha Wadau amewapongeza viongozi  wa Serikali kwa kutambua umuhimu wa kufanya kazi na viongozi wa Dini  kushirikishwa katika mambo ya kiserikali.

Hata hivyo ametoa rai kwa wananchi kuwa siku ya Mkesha wa Mwenge wa Uhuru wananchi wawe na maadili ili kuhakikisha zoezi hilo linaenda vizuri.

Kutoka kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Machi 14,2022.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa