• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

wasimamizi wa uchaguzi Madaba wapewa mafunzo ya uchaguzi

Posted on: October 26th, 2020

MSIMAMIZI wa Uchaguzi Jimbo la Madaba mkoani Ruvuma Shafi Kassim Mpenda ametoa rai kwa Makarani waongozaji  na wasimamizi wa Uchaguzi Mkuu  kuwapa kipaumbele watu wenye makundi maalum siku ya uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 28,2020.

Ametoa rai hiyo wakati anafungua mafunzo hayo katika ukumbi wa shule ya Madaba day iliyopo katika Kata Mkongotema Halmashauri ya Madaba .

Mpenda ametoa rai kwa Makarani  waongozaji na wasimamizi kuwa  waadilifu katika majukumu yao kwa  kutoshabikia chama chochote wakiwepo kwenye kituo cha uchaguzi ili kulinda amani ya Tanzania.

‘’Wapo Mawakala wa vyama vya Siasa wapo kwaajili ya kusaka kura na kuna vyama 15 vilivyoshiriki uchaguzi kupigania au kulinda maslahi ya chama husika, isiwe sehemu ya kujenga urafiki na mawakala,wala mchakato wowote kwaajili ya mgombea wa chama chochote”.

 Mpenda amewahakikishia Makarani waongozaji na Wasimamizi wa vituo usalama wawapo kazini siku ya uchaguzi na kuhakikisha wanawahudumia wananchi wote kwa usawa bila upendeleo.

Amewasisitiza Makarani waongozaji na wasimamizi wa vituo  kuwa uchaguzi ni moja ya mambo manne nyeti kama vile Mitihani,Mwenge,Ziara za viongozi wa Serikali hivyo amesema kila mmoja ahakikishe anakuwa na nidhamu awapo katika kituo cha kupigia Kura.

Mwenyekiti wa Mafunzo hayo Denis Ngwahi  amewaomba makarani wa uchaguzi kufanya kazi kwa umakini na kutofanya kazi kwa mazoea kwa sababu Tume ya uchaguzi wamewaamini.

Naye Msimamizi Mkuu Kata ya Lituta  Agatha Ngunga kwa niaba ya wenzake amewaahidi kuwa uchaguzi utakuwa wa amani na watafuata maelekezo yote waliyopatiwa kwenye mafunzo hayo .

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Afisa Habari Halmashauri ya Madaba

Oktoba 26,2020.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa