• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MKUU wa Mkoa Ruvuma azindua Kumbukizi la Mashujaa wa Majimaji

Posted on: February 24th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amezindua kumbukizi la miaka 115 ya mashujaa wa vita ya Majimaji na tamasha la utalii wa utamaduni lililofanyika kwenye viwanja vya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji Mahenge Songea 

Uzinduzi huo umefanyika katika viwanja vya Mashujaa ya majimaji vilivyopo Manispaa ya Songea amesema Februari 27, 1906 mashujaa wapatao 67 walinyongwa na wakoloni wa Kijerumani.

Ibuge amewaasa wananchi wa Mkoa huo kuendelea kuwaenzi mashujaa hao kwa kuwa walijenga msingi muhimu wa kupiga vita ukoloni na ubeberu  dhidi ya nchi yetu ya Tanzania ikiwemo mikoa ya kusini.

”Kumbukizi ya Februari 27 kila mwaka inatoa fursa kwa Wananchi wa Tanzania na hususani Mkoa wa Ruvuma kuendeleza urithi wa utamaduni wa asili kwaajili ya vizazi vya sasa na vijavyo”.

Hata hivyo amesema kumbukizi hiyo inasaidia kuibua na kuendeleza fursa za utalii wa utamaduni wa Mkoa wa Ruvuma na Ukanda wa Kusini ili kuinua uchumi na kuboresha hali ya maisha ya wananchi.

“Serikali kwa lengo la kutambua na kuendeleza mchango  wa Wajasiliamali na taasisi za serikali kwa kukuza uchumi kwa vitendo maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu Sera ya Tanzania ya Viwanda pamoja na kukuza utalii Ukanda wa Kusini”.

Mhifadhi wa Makumbusho ya Majimaji Batazar Nyamsya amesema vita hivyo vilitokea Julai 1905 mpaka 1907 Agosti na viongozi walioshiri katika vita hivyo walihukumiwa kunyongwa mpaka kufa Februari 27 1906.

Amesema wazo la maadhimisho hayo ilianzishwa na wazee wa Kingoni walitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa Martini Haule aliyekuwa ameteuliwa wakati huo na alichukua hatua ya dhati katika kushughulikia jambo hilo.

Nyamusya  vifaa vya awali katika Makumbusho haya vilikusanywa na Mh.Dkt .Laulence Mtazama Gama padre chengula na baadhi ya wazee na kufufuliwa rasmi Julai 6,1980.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Ofisi ya Hbari ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Februari 23,2022

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa