• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika

MKUU wa JKT ampongeza Mkoa wa Ruvuma kwa kuongoza katika uzalishaji wa Chakula

Posted on: September 16th, 2023

MKUU wa Jeshi la Kujenga Taifa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele  ameupongeza Mkoa wa Ruvuma kwa kuongoza kwa uzalishaji wa mazao ya nafaka nchini hivyo kuchangia pato la Mkoa kwa asilimia 75.

Meja Jenarali Mabele ametoa pongezi hizo wakati anazungumza na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas alipomtembelea ofisini kwake mjini Songea katika ziara ya kikazi mkoani humo.

“Niwapongeza Mkoa wa Ruvuma mimi nilikuwa Mbeya  wakati mnakabidhiwa  na Mheshimiwa Rais Tuzo ya mzalishaji wa kwanza wa mazao ya nafaka nchini,katika mikoa yote ninyi mlionekana mmefanya vizuri zaidi kwenye kilimo’’,allisisitiza.

Hata hivyo alisema anaamini Jeshi la Kujenga Taifa kambi ya Mlale  wilayani Songea ,ni sehemu ya wazalishaji wa mazao ya nafaka hivyo katika tuzo iliyotolewa JKT Mlale pia wametoa mchango.

 Amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kwa kutoa ushirikiano mkubwa katika kambi ya JKT Mlale ambapo amemuomba Mkuu huyo wa Mkoa kuendelea kuwatumia vijana wa JKT katika shughuli mbalimbali.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas  amesema katika msimu wa mwaka 2022/2023 Mkoa wa Ruvuma umezalishaji tani 1,598,163 za mazao ya chakula hali iliyosababisha Mkoa kuwa na ziada ya chakula tani 1,043,525.

Hata hivyo amesema kati ya tani hizo zao la mahindi pekee zimezalishwa tani 1,043,324 na kwamba wananchi 1,848,794 waliopo mkoani Ruvuma wanahitaji chakula tani 554,638 hivyo Mkoa kuwa na ziada kubwa ya chakula.Pichani katikati ni Mkuu wa Jeshi ;la Kujenga Taifa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele akipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas mwenye suti ya bluu alipofika ofisini kwa Mkuu huyo wa Mkoa mjini Songea

Asilimia 87 ya wakazi wa Mkoa wa Ruvuma wanategemea kilimo.Kwa mwaka wanne mfululizo Mkoa wa Ruvuma unaongoza kwa uzalishaji wa mazao ya nafaka nchini.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • RAIS Samia atoa Milioni 90 ukarabati wa Madarasa 6 Ifinga

    September 24, 2023
  • MWENYEKITI Madaba aagiza kuezeka Kituo cha Afya Ifinga Mara Moja

    September 24, 2023
  • WANANCHI Lilondo wajitolea kujenga Nyumba 6 za walimu

    September 23, 2023
  • WANANCHI Ifinga walivyojiwekea benki tofari 400,000 kwaajili ya Ujenzi wa Miradi ya Serikali

    September 23, 2023
  • Angalia zote

Video

MADIWANI MADABA WAADHIMIA KUSIMAMIA MIRADI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 10

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: info@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa