• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MKOA wa Ruvuma watenga ekari 48,343.35 kwaajili ya kilimo cha Mkataba

Posted on: October 27th, 2021

MKOA wa Ruvuma umetenga jumla ya  ekari 48,343.35 za ardhi kwa ajili ya kilimo cha pamoja na Mkataba kwa zao la Alizeti,Ufuta na Soya ikiwa ni mkakati wake wa kutaka kujitosheleza kwa mafuta ya kula.

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amesema hayo jana,wakati akifungua Mkutano wa wadau  wa kilimo uliohudhuriwa na Wakuu wa wilaya,Wakurugenzi wa Halmashauri,maafisa ugani na taasisi za fedha.

Aidha amesema, mkakati huo unakusudia na utasaidia  Taifa kuepuka kutumia  fedha nyingi kuagiza bidhaa hiyo nje ya nchi na kuinua vipato vya wakulima na Nchi kwa jumla.

Ameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kutenga Sh.bilioni 2.2 kwa ajili ya ununuzi wa mbegu bora za Alizeti ambazo awali zilikuwa zikiuzwa na wafanyabiashara kwa bei ya Sh.35,000 kwa kilo.

Ibuge amesema,kupitia mpango huo sasa mbegu za alizeti  zitauzwa kwa bei ya Sh.3,500 kupitia wakala wa mbegu(Asa) sawa na asilimia kumi ya  bei ya awali  na kuwasihi wananchi wa mkoa wa Ruvuma kutumia fursa hiyo kuwekeza katika kilimo cha zao hilo.

Amesema,katika mkoa wa Ruvuma mahitaji ya mbegu za alizeti,soya na ufuta ni  kilo 310,222 na mbolea ni tani 1,662 ambapo kwa msimu wa kilimo 2021/2022 Halmashauri za mkoa huo zimepanga kulima ekari 12,570 kati ya ekari 48,343 zilizotengwa.

Amesema, ekari hizo zitahitaji tani 112  ambapo zao la ufuta mahitaji ni tani 21,soya tani 77 na alizeti tani 14,na kuzielekeza Halmashauri kuhakikisha zinawezesha upatikanaji wa mbegu na pembejeo hizo kwa wakati ili wakulima wasikwame.

Pia amesema, katika msimu wa kilimo 2021/2022 mkoa huo umejipanga kutekeleza mfumo wa kilimo cha pamoja na kilimo cha mkataba(Block Farming& Contract Farming) kwenye Halmshauri ambacho kinahusisha utengaji wa maeneo  kwa wakulima hulima eneo moja.

Amesema, kilimo hicho wakulima watapata huduma za ugani na urahisi wa upatikanaji wa pembejeo na masoko ambapo wahusika wa mpango huo ni Vyama vya Ushirika,wakulima,vikundi,taasisi mbalimbali za umma na binafsi na makampuni ya ndani nan je ya Nchi.

Kwa mujibu wa Jenerali Ibuge,Serikali ya mkoa imeridhia kilimo hicho cha mktaba kwa wakulima kinachohusisha makubaliano baini ya mkulima na kampuni au mtoa huduma ambaye atahusika kutoa pembajeo,huduma ya ugani na ununuzi wa mazao  kwa lengo la kuinua kipato.

Katika kikao hicho, Ibuge ameziagiza Halmashauri kwenda kuviwezesha vikundi vitakavyohitaji kuwekeza katika mazao hayo, na kuhakikisha wanatenga eneo angalau moja  kwa ajili ya taasisi ya utafiti wa kilimo(Tari) ambalo litatumika  kama shamba darasa na kuzalisha mbegu bora kwa mazao ambayo Halmashauri itaanza nayo.

Kwa upande wake Katibu Tawala msaidizi uchumi na uzalishaji Jeremiha Sendoro amesema, manufaa ya kilimo cha pamoja ni kutumia rasilimali  kidogo kama maafisa ugani wachache kuwafikia wakulima wengi na kalenda ya kuhudumia shamba huandaliwa kwa pamoja.

Sendoro ametaja faida nyingine, ni  usambazaji wa pembejeo hufanywa  kwa urahisi kwa kuwa mashamba yote yapo kwenye uelekeo mmoja na upatikanaji wa masoko ni rahisi kwa sababu mazao ukusanywa kwenye maghala au soko moja.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa