• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MKOA wa Ruvuma waridhia kupandisha hifadhi mbili za misitu ya asili

Posted on: June 10th, 2021

MKOA wa Ruvuma umeridhia kupandisha hadhi Hifadhi mbili za misitu kuwa mapori ya akiba (Game Reserve) kwa lengo la kuboresha sekta ya utalii kusini.

Mshauri wa Maliasili na Utalii Mkoa wa Ruvuma Afrikanus Challe ameyataja mapori hayo kuwa ni Gesimasowa lenye ukubwa wa kilometa za mraba 764 lililopo Halmashauri ya Madaba wilayani Songea na pori la Litumbandyosi lenye ukubwa wa kilometa za mraba 494 lililopo wilayani Mbinga.

“Mapori yote mawili ni sehemu ya ekolojia ya ushoroba wa Selous-Niassa,hata hivyo hadi sasa bado hifadhi  hizo haziajapata Tangazo rasmi la serikali la kuwa ni mapori ya akiba,ingawa mchakato wa kutangaza upo katika hatua za mwisho’’,alisisitiza.

Challe amesema Mkoa wa Ruvuma,una mpango wa kuanzisha mashamba ya wanyapori katika Jumuiya zote tano za uhifadhi,kikiwemo kisiwa cha Lundo ndani ya ziwa Nyasa na katika chuo cha Maliasili cha Likuyusekamaganga wilayani Namtumbo ili wananchi wajifunze na kuanzisha mashamba binafsi ya wanyamapori.

Akizungumzia fursa za utalii zilizopo katika Mkoa wa Ruvuma,amesema Mkoa una fursa za utalii wa kiutamaduni na kiikolojia ambapo amezitaja baadhi ya fursa hizo kuwa ni mapori ya akiba ya Selous,Mwambesi,ziwa Nyasa lenye samaki wa mapambo,visiwa,fukwe za kuvutia na vuvutio vingine lukuki.

Fursa nyingine amezitaja kuwa ni mto Ruvuma wenye maporomoko ya Nakatuta,Tulila na Sunda ambayo yamekuwa yanavutia watalii wengi wa ndani na nje ya nchi.

Challe amezitaja fursa za utalii wa kiutamaduni kuwa ni majengo ya kihistoria yakiwemo makanisa makongwe ya Peramiho,Lituhi na Lundu, makumbusho ya vita ya Majimaji,historia ya machifu wa kiyao,wangoni na historia ya biashara ya utumwa.

Fursa nyingine za utalii wa kiutamaduni amezitaja kuwa ni historia ya wapigania uhuru  wa Afrika,jiwe la Mbuji,mapango ya wamatengo na pango la mlima Chandamali ambalo lilikuwa maficho ya Nduna Songea Mbano wakati wa Vita ya Majimaji.

Ili kuhakikisha vivutio vilivyopo vinaleta tija,Challe amesema Mkoa umeendelea kufanya jitihada za kuboresha miundombinu na matangazo katika vyombo vya habari ambayo yatawezesha fursa hizo kufahamika kitaifa na kimataifa.Ameipongeza serikali kuu kwa kuboresha miundombinu ya barabara na anga hivyo kuvutia watalii na kuufungua Mkoa na ukanda wa kusini katika sekta ya utalii na uwekezaji.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Juni 9,2021

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa