• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MKOA wa Ruvuma wapanda Miti Milioni 2.4

Posted on: February 22nd, 2022

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amezindua upandaji wa miti katika Halmashauri ya Madaba Wilaya ya Songea.

 Ibuge amesema tangu kuanza kwa mvua za masika Januari mwaka huu hadi sasa katika Mkoa imepandwa miti Zaidi ya milioni 2.4.

Ibuge ameyasema hayo wakati anazungumza baada ya kuzindua upandaji miti kwenye vyanzo vya maji kimkoa katika kijiji cha Mwande Kata ya Matetereka Halmashauri ya Madaba.

“Maelekezo niliyoyatoa siyo ya Mkuu wa Mkoa bali ni ya kitaifa kutoka kwa Mh. Rais na Makamu wa Rais ndiye anayesimamia mazingira ni mkakati lazima tuzingatie kwa kuhakikisha kila Halmashauri angalau kwa mwaka inapanda miti milioni 1.5’’.

Ibuge amesema miezi mitatu iliyopita ametembelea vyanzo vya maji amejionea uharibifu mkubwa wa ukataji wa miti hivyo ametoa rai kwa wananchi wote wa Mkoa kurejesha hali ya uoto wa asili ili kuwa na uhakika wa mvua na kulinda mazingira.

Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololeti Mgema katika uzinduzi huo amesema suala la upandaji wa miti limeshirikishwa katika Taasisi na Shule mbalimbali pamoja na wananchi wote wa Wilaya hiyo.

Afisa misitu Shamba la Miti la Wino Grory Kasmir katika zoezi la upandaji Miti amesema kufuatia maelekezo ya Mkuu wa Mkoa wamefanya vikao na viongozi wa Wilaya ,RUWASA, pamoja na wananchi  kuweka makubaliano ya kuhakikisha vyanzo vya maji wanaunda vikundi vya kulinda vyanzo vya Maji.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Ofisi ya Habari ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Februari 22,2022.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa