• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MKOA wa Ruvuma wakusanya mapato ya ndani asilimia 134

Posted on: February 21st, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas  ameipongeza Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) kwa kufanikiwa kukusanya mapato ya ndani zaidi ya shilingi bilioni 29.5 sawa na asilimia  134 katika kipindi cha mwaka 2022/2023.

Kanali Thomas ametoa pongezi hizo wakati anazungumza kwenye ufunguzi wa Kikao cha Baraza la Ushauri la Mkoa (RCC) kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Amesema TRA katika kipindi hicho wamefanya kazi nzuri ya kukusanya mapato kwa kuwa wamevuka lengo la makusanyo ya zaidi ya shilingi bilioni 21 ambapo amesema Uchumi wa Mkoa wa Ruvuma umeendelea kuimarika.

“Mkoa unaendelea kuimarika kiuchumi kwa kuimarika kwa miundombinu,shughuli za uzalishaji mali,biashara na ukewekezaji shughuli za uchimbaji madini hasa makaa ya mawe,maboresho ya uwanja wa Ndege wa Songea na biashara na nchi jirani za Msumbiji na Malawi’’,alisistiza RC Thomas.

Ameyataja mazingira ya kujifunzia na kufundishia  wanafunzi yamekuwa bora zaidi ambapo Mkoa uliletewa fedha za kujenga shule mpya 12 za msingi kupitia BOOST kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 7,7 pia serikali ilileta fedha zaidi ya shilingi bilioni tano kujenga sekondari mpya tisa kupitia program ya SEQUIP.

Kulingana na Mkuu wa Mkoa katika kipindi cha mwaka 2022/2023 serikali imetoa shilingi milioni 900 kukarabati hospitali kongwe ya Tunduru na zaidi ya shilingi bilioni tatu zimetolewa na serikali  kujenga hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma katika eneo la Mwengemshindo Manispaa ya Songea.

Ameongeza kuwa serikali imetoa shilingi bilioni 9.3 kujenga vituo vya afya 14  na kwamba serikali imenunua mashine ya CT scan na digital xray kwa ajili ya hospitali ya Rufaa ya Mkoa na mashine ya Xray kwa ajili ya hospitali ua Halmashauri ya Madaba.

Akizungumzia sekta ya kilimo,Mkuu wa Mkoa amesema serikali imeingiza mbolea ya ruzuku mkoani Ruvuma jumla ya tani 90,000  ambapo hadi sasa mbolea tani 62,540 zimesambazwa kwa wakulima.

 Maazimio yaliyopitshwa katika kikao hicho cha RCC ni Pamoja na kila halmashauri kutumia mapato yake ya ndani kujenga shule ya bweni ya wavulana na wasichana na kufanya ufuatiliaji wa ujenzi wa chuo cha SUA tawi la Tunduru.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa