• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MKOA wa Ruvuma kitato cha sita kufikia asilimia 98

Posted on: January 14th, 2021

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amewapongeza wadau wa Elimu kwa  kiwango cha ufaulu wa matokeo ya kidato cha sita mwaka 2020 umefikia asilimia 98.68.

Akitoa taarifa hiyo wakati akifungua Kikao cha kamati cha Ushauri wa Mkoa amesema hali ya ufaulu katika mitihani ya Kitaifa ya Elimu ya Msingi na Sekondari mwaka 2020 matokeo yalikuwa asilimia 78.52,mwaka 2019 ufaulu ulikuwa asilimia 83.70.

“Naipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kufaulisha kwa asilimia 85.51 na inatakiwa kuongeza juhudi ili kupandisha ufaulu zaidi kwani matokeo yanaonyesha wamefaulu kwa asilimia 66.68”.

Mndeme amesema katika kikao hicho miundombinu kwaajili ya Wanafunzi wa kidato kwanza 2021,Takwimu inaonyesha hadi kufikia Novemba 2020 kulikuwa na upungufu wa vyumba 43 kwaajili ya kidato cha kwanza.

“Nimetoa maelekezo kwa Halmashauri zote kuhakikisha wanafunzi wote waliofaulu wanaanza masomo Januari 2021,Tumejipanga vizuri hakuna mtoto atakaebaki nyumbani kwa kukosa nafasi na Mkoa wetu ni kati ya Mikoa 9 nchini ambayo wanafunzi wote waliochaguliwa kuanza kidato cha kwanza watapata nafasi.

Hata hivyo Mndeme  amesema Mkoa unatekeleza Kampeni ya Magauni manne chini ya Kaulimbiu ya Niache Nisome,ambapo Serikali ya Mkoa wa Ruvuma kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa Elimu inapambana na kuhakikisha inaondoa vikwazo vinavyosababisha wanafunzi wa kike kushindwa kuhudhuria masomo.na kumaliza.

Amesema Vikwazo hivyo ni pamoja na Mimba za utotoni hali inayosababisha wanafunzi wakatishe masomo na kufifisha ndoto zao.

Mkuu wa Mkoa amesema katika kupambana na kikwazo Mkoa kupitia Halmashauri zake umejenga Shule za wasichana  pamoja na kujenga Hostel kwa shule za kutwa ili kuwasaidia wanafunzi wa kike kuepuka vikwazo hivyo.

Amesema shule hizo zimejengwa katika Halmashauri zote za Mkoa wa Ruvuma isipokuwa Halmashauri ya Madaba,Kamati ya Ushauri ya Mkoa imeona umuhimu wa kujenga Shule ya Sekondari ya Wasichana katika Halmashauri ya Madaba itakayo chukua wanafunzi kutoka maeneo yote ya Mkoa.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Afisa habari Halmashauri ya Madaba

Januari 14,2021

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa