• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MKAA mbadala kuongeza pato la Taifa asilimia 2.5

Posted on: July 31st, 2021

WAZIRI wa Maliasili na Utalii Damasi Ndumbaro amezindua Mkakati wa utekelezaji wa Sera ya Misitu na Utiaji sahihi kanuni za uendelezaji wa Nishati ya Mkaa Mbadala.

Uzinduzi huo   umefanyika katika Viwanja vya Majimaji Manispaa ya Songea  katika Tamasha la Majimaji Selebuka na kauli mbiu imekuwa Misitu ni uchumi tumelithishwa tuwalithishe.

Amesema Misitu inamuhimu katika maisha ya mwanadamu inasaidia kutuletea mvua,na nyuki ikiwemo katika tamasha hilo umefanyika uzinduzi wa Nyuki Duniani na kuzinduliwa na Waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda .

“Misitu ni chanzo cha nishati wengi tunatumia kuni kwenye kupika na mkaa unaotokana na misitu, ipo mikaa ya aina nyingi lakini wataalamu wametuambia kuna mkaa mbadala  unaotengenezwa kupitia mazao ya misitu na kilimo ni muhimu katika nuchumi wanchi na kutoa ajira”.

Hata hivyo Ndumbaro amesema Mkaa huo ulikuwa hautendewi haki wataalamu baada ya kufanya utafiti wamegundua mkaa huo mbadala kuuzwa mpaka nchi za nje na kupata faida kubwa.

Ndumbaro akizungumzia mkakati wa sera ya misitu,kuhakikisha watanzania wanatumia mkaa mbadala ili kuweza kuokoa Misiti na kutunza mazingira na kujipatia kipato.

“Mkaa huo mbadala unatokana na mabaki ya miti,pumba za mpunga,malanda ya mbao,mabua ya mahindi na takataka  hata sasa kunawafanyabiashara 19 wameanzisha viwanda vya kutengenezea Mkaa nchini na baada ya kusainikanuni hizo watasafirisha mkaa wao nchi za nje na kuchangia pato la taifa, sekta ya misitu inaingiza asilimia 3.5 na mkaa na kuni  huingiza 1.5 baada ya kuzindua mkakati huo tunatarajia kuingiza 2.5 mkaa na kuni “.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii Dr. Ezekiel Mwakalukwa amesema utekelezaji  wa Taifa wa sera ya misitu wa mwaka 1998 na mkakati wa miaka 10 kuanzia  2021 mpaka 2031,na kuongozwa na sera ya Taifa ya mwaka 1998 inamiaka 23 sasa tangia imeanza.

Mwakalukwa amesema utekelezaji wa sera hiyo umekuwa umekuwa ukitekelezwa kuanzia mwaka 2001 mpaka 2010 na mpango ulipomalizika ilikosa mwongozo wa kuongoza utekelezaji wa malengo ya sera ya Taifa ya Misitu.

“Kutokana na hatua hiyo Wizara ya Maliasili na Utalii iliunda kikosi kazi kwaajili ya kufanya tathimini  ya kina ya sera ya Taifa ya mwaka 1998 kama malengo yaliyopo katika Sera hiyo yanatosha na kufikia uhifadhi endelevu katika Sekta ya Misitu nchini”.

Mkurugenzi amesema baada ya kupitia sera hiyo ilionekana kuwa bado inaweza kutumika na kuongoza Sekta ya misitiu mwaka 2020 Wizara ya Maliasili iliunda kikosi kazi kingine na kuandaa rasimu ya mkakati huo na kupiwa na wadau mbalimbali kwa kutoa maoni na katika warsha mbalimbali na kamati ya mazingira

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Afisa Habari Halmashauri ya Madaba

Julai 30,2021

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa