• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MENEJA TFS Wino atoa rai siku ya Mtoto wa Afrika kwa wazazi Kuacha kuwatuma usiku

Posted on: June 17th, 2023

WADAU  mbalimbali Halmashauri ya Madaba wamejitokeza kutoa Zawadi kwa Wanafunzi Siku ya Maadhimisho ya Mtoto wa Afrika

Meneja wa Shamba la Miti Wini Grory Kassmir akizungumza katika maadhimisho hayo amesema kwa kushirikiana na Jamii wamemuunga Mkono Mwenyekiti wa Halmashauri na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kushiriki siku hiyo na kutoa Zawadi kwa Watoto.

“Kama Wakala wa Shamba la Miti Tanzania kwa upande wa Shamba la Miti Wino tumeleta Sabuni,taulo za kike,Sukari kilo 50,Daftari,Kalamu za Wino na Penceli.

Kassmiri amewaasa watoto wajifunze kusema hapana pamoja na kujiepusha na mazingira hatarishi ikiwa wazazi waache kutuma watoto usiku.

“Tuwe kama wazazi wa zamani ukimuona mtoto mwambie ondoka uende nyumbani lakini watoto wengi wanaharibika kwa kuzunguka usiku’’.

Mwenyekiti wa Halmashauri Teofanes Mlelwa amesema wapo na mashirika mbalimbali wamekuja na zawadi lakini kimsingi siyo zawadi ni haki yao hivyo wanakumbushwa kufanya hivyo mara nyingi.

Mlelwa amesisita na kuwaasa  jamii kuwatunza watoto kama walivyoandika na kudai haki katika mabango yao, Kwa kupatiwa haki ya msingi ya Elimu,kupatiwa Afya ,haki ya kusikilizwa pamoja na malazi.

Hata hivyo katika maadhimisho hayo watoto wa shule ya Msingi Matetereka waamepewa zawadi mbalimbali ikiwemo taulo za kike,madaftari,peni,kalamu,mafuta ya kupaka,sukari na sabuni.

Amesema vifaa hivyo vimetolewa na wadau mbalimbali ikiwemo ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Madaba,Ofisi Shamba la Miti Wino(TFS),NMB Madaba,Mkinga Foundation Pamoja na Kikundi cha Bodaboda konabar.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Juni 16,2023.                   

 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa