• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MBIO Maalum za Mwenge wa Uhuru kufungua miradi 34 yenye thamani ya zaidi ya bilioni 12 Ruvuma

Posted on: September 1st, 2021

JUMLA ya miradi  34 yenye thamani ya Sh. Bilioni 12,626,057,642.40  inatarajiwa kufikiwa na Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka  2021 iliyotekelezwa na Serikali na kusimamiwa na wananchi katika mkoa wa Ruvuma.

Mkuu wa mkoa huo Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amesema hayo leo(jana) wakati akiongea na waandishi wa Habari Ofisini kwake ambapo ameeleza kuwa,kati ya  hiyo miradi miradi kumi yenye thamani bilioni 2,629,431,922.61 itazinduliwa.

Aidha ametaja,miradi minne yenye thamani ya Sh. Milioni 439,945,705.37 itafunguliwa,miradi minane yenye thamani ya Sh. Bilioni 8,192,394,296.40 itawekewa jiwe la msingi na miradi kumi na sita yenye thamani ya Sh. Bilioni 1,364,285,718.02 itatembelewa na kukaguliwa pamoja na kugawa vifaa mbalimbali.

Mkuu wa mkoa amesema,  Mwenge wa Uhuru ukiwa mkoani Ruvuma utakimbizwa katika wilaya zote tano kuanzia kesho tarehe 2 Agosti hadi tarehe 6 kwa umbali wa km 1,055.1.

Ujumbe wa Mwenge wa Uhuru mwaka 2021 umebeba  ujumbe unaojikita katika umuhimu wa TEHAMA kwa maendeleo endelevu ya Taifa letu ambao unawakumbusha na kuwataka Wananchi  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutumia maendeleo ya Tehama kwa usahihi.

Brigedia Jenerali Ibuge amesema, mkoa wa Ruvuma una shauku  na ari kubwa ya kuupokea  na kuukimbiza Mwenge wa Uhuru ili kutimza malengo yake.Pia,amewakumbusha wananchi wote kuendelea kuchukua tahadhari ya ugonjwa wa Uvico 19 kwa kuvaa Barakoa  muda wote wawapo kwenye mikusanyiko,kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni na kutumia vipukusa mikono mara kwa mara.

Brigedia Jenerali Ibuge amesema, katika maeneo yote ya mkesha wa Mwenge,zoezi la utoaji chanjo ya Uvico -19 kwa hiari litaendelea.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Septemba Mosi,2021

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa