• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MAHAFARI ya Kidato cha nne Madaba day yalivyopendeza

Posted on: September 30th, 2023

WANAFUNZI 103 Katika Shule ya Sekondari ya Madaba day wanatarajia kuhitimu Kidato cha Nne mwaka 2023 katika Halmshauri ya Madaba.

Mkuu wa Shule Kelvin Kalesa akisoma taarifa katika Mahafari ya 22 yaliyofanyika Shuleni hapo amesema shule hiyo ni ya kutwa inawanafunzi 758 ikiwa kidato cha kwanza hadi kidato cha nne ni mchanganyiko wa wasichana na wavulana na kidato cha tano na sita wavulana pekee.

Kalesa amesema shule hiyo ilianza Mwaka 1996 ikijengwa kwa nguvu za wananchi mwaka 2002 Shule ilichukuliwa na Serikali na kupewa namba ya Usajili S.88 na kituo cha mtihani S.1199.

Amesema Shule hiyo inajumla ya Walimu 29 ikiwa wanaume 20 ni wanawake  9 na wafanyakazi wasio walimu 10.

Mkuu wa Shule amezitaja changamoto zilizopo shuleni hapo ikiwemo uhaba wa viti na meza kwaaajili ya Walimu na wanafunzi,Ukosefu wa Hosteli ya kidato cha kwanza hadi kidato cha nne.

“Mabweni yaliyopo yanatumiwa na kidato cha tano hadi cha sita yalijengwa na wananchi kwaajili ya kidato cha kwanza hadi nne”.

Amesema changamoto nyingine ni uchakavu wa madarasa yanayoonyesha kama shuleni hapo kuna shule mbili tofauti kuna madarasa ya kisasa na madarasa ya zamani.

Kwaupande wake Mgeni rasmi Mbunge waJimbo la Madaba Joseph Mhagama akiwakilishwa na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Olaph Pili amewaasa wanafunzi hao kuhakikisha wanasoma kwa mda mchache uliobaki na kuepuka kufeli na kupata Mimba za utotoni zitakazopelekea kuharibu ndoto kwa wanafunzi hao.

Pili ametoa rai kwa wazazi kuendelea kuchangia chakula cha wanafunzi Shuleni kwa hiyali ikiwa ni Sera ya Serikali na niwajibu wa kila mzazi kuchangia.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri amejibu lisala hiyo kwa niaba ya Mbunge amesema tatizo la uchakavu wa Madarasa na ukosefu wa hosteli wamelichukua watalifanyia kazi.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Septemba 30,2023.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa