• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MADIWANI Madaba wapewa Mafunzo ya Maadili

Posted on: January 31st, 2024

MADIWANI Halmashauri ya Wilaya ya Madaba wamepewa mafunzo ya Maadili ya Uongozi katika kikao cha Baraza la Madiwani cha robo ya Pili 2023.

Akitoa mafunzo hayo afisa wa Maadaili kutoka ofisi ya viongozi wa maadili  kanda ya Kusini Samweli Omary amesema Maadili ni kufanya kilicho sahihi iwe ni kwa kunena au kwa kutenda kwa mujibu wa sheria kanuni na taratibu zilizowekwa.

“Kama viongozi na watumishi wa umma mliopo katika ukumbi huu tunaendelea kuwahimiza kuwa waadilifu kwa kuzingatia sheria,kanuni na tarabitu na miongozo mbalimbali kila mmoja katika eneo lake”.

Hata hivyo Omary amesema kwa kila kiongozi ahakikishe anazingatia miongozo na kanuni za Nchi iliyowekwa na kiongozi akifanya tofauti na hapo atatafsiliwa amekiuka maadili.

Amesema Maadili yanasaidia kuchambua na  kupambanua mambo mema na oevu mazuri na mabaya yanayokubalika na yasiyokubalika,yanayositirika na yasiyositirika na kuwezesha kufanya mambo sahihi kwa wakati wowote na mahali popote.

Mtu mwadilifu anapimwa kwa jinsi ambavyo anadumisha ushirikiano kwa watu au jamii inayomzunguka kwa kudumisha umoja na wale ambao anafanyanao kazi au jamii anayoiongoza.

“Madiwani,Wakuu wa Idara na watumishi wenzangu lazima tuonyeshe tunazingatia umuhimu wa maadili kwenye utumishi wa Umma tunaongozwa na Sheria kanuni taratibu na miongozo hata kwenye jamii ndio mana zipo sheria”.

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmshauri ya Wilaya ya Madaba

Januari 31,2024.      

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa