• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MADABA wataja mafanikio ya utoaji wa Elimu ya Lishe kwa Jamii

Posted on: October 26th, 2023

HALMASHAURI ya Wilaya ya Madaba  kupitia kitengo cha Lishe kwa mwaka wa fedha 2022/2023 wamefanikiwa kutoa Elimu ya lishe katika Kata na Vijiji .

Akitoa taarifa hiyo Afisa Lishe wa Halmashauri hiyo Joseph Peter katika Kikao cha Tathimini ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe, robo ya kwanza 2023/2024.

Peter amesema mafanikio hayo ni pamoja na kutoa Elimu ya Unyonyeshaji kwa wazazi wenye watoto chini ya miaka 5 wapatao 486 katika Zahanati ya Magingo,Hanga Ngadinda na Maweso na kutoa matibabu ya Utapiamlo kwa watoto 4.

Amesema wamefanikiwa kuwajengea uwezo waratibu wa Lishe  ngazi ya Vituo wapatao 21 ya masuala mbalimbali,ukaguzi wa vyakula katika maduka ya vyakula 30 katika Kata ya Lituta na Mahanje.

Hata hivyo Afisa Lishe amesema changamoto zinazowakabili wananchi ikiwa msimu wa kilimo wazazi wengi kuhamia mashambani na kuacha kuzingatia malezi ya watoto pamoja na wajawazito kupelekea kuathiri afya zao.

Kutowafanyia mafunzo rejea kwa masuala ya Lishe kwa wahudumu wa afya ngazi ya jamii ambapo kupelekea kuathiri utoaji wa huduma sahihi za Lishe.

Peter ameelezea mikakati ya kutatua changamoto hizopamoja na  kuendelea kutoa Elimu ya lishe na malezi na mafunzo kwa jamii ili kuhakikisha watoto na wajawazito  wanakuwa na hali nzuri ya lishe.

“Halmashauri kutenga fedha kupitia mapato ya ndani kwa mwaka wa fedha 2024/2025 ili kufanya mafunzo rejea kuwajengea uwezo wahudumu wa afya ngazi ya jamii”.

Amesema kuendelea kufanya maadhimisho ya Siku ya Afya na Lishe ya kijiji, kuimarisha utoaji wa Elimu pamoja na Halmashauri kuunda klabu za Lishe kwa wanafunzi  na kuhamasisha utekelezaji wa shughuli za lishe.

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Oktoba 25,2023.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa