• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MAAFISA Ustawi na Maafisa Lishe watoa Elimu siku ya Mtoto wa Afrika

Posted on: June 17th, 2023

KUFUATIA Maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika Afisa Ustawi wa Jamii Shani Kambuga na Afisa Lishe John Mapunda Halmashauri ya Madaba wametoa Elimu kwa Jamii.

Afisa ustawi amesema kuna taasisi tatu ikiwemo ngazi ya familia inayohakikisha watoto wanalelewa ambayo inaishi  na watoto kwa Mda mwingi hivyo Familia ikilegalega watoto hawawezi kupata haki yao ya msingi.

Kambuga amesema Taasisi ya Pili ni jamii ambayo kimsingi inatakiwa kuhakikisha mtoto analindwa na kuwalea pamoja na kuwatunza, jamii ikipuuzia husababisha ukatili wa watoto ikiwa Taasisi ya tatu ni Serikali inawajibika kuwatunza na kuwalea watoto hao.

“Wananchi tunawaombeni sana Familia,Jamii pamoja na Serikali tuungane ili tuweze kuwalea watoto kwa pamoja kwa malezi bora hao ndio Taifa letu la Kesho Mh. Rais Samia amekuwa akisisitiza sana kupinga ukatili dhidhi ya watoto”.

Kwa upande wake Afisa Lishe John Mapunda amesema kupitia siku ya mtoto wa Afrika idara ya Afya wamekuwa na jukumu la kusimamia haki ya  msingi ya mtoto kwa kupatiwa Matibabu na Lishe.

Mapunda amesema kwa kutambua hivyo wanasimamia mpango wa Serikali wa 2021 mpaka 2026 jukumu kubwa kuzuia tatizo la upungufu wa uzito hasa kwa watoto na tatizo la ukosefu wa Madini na vitamini.

“leo katika banda letu tunatoa huduma ya matone ya vitamini A  kwa watoto chini ya miaka 5 na tathimini ya hali ya Lishe kwa watoto kuanzia miaka 5 hadi 18”.

Amesma wanafanya hivyo kwa lengo la kujua hali zao kwa sababu wapo katika misingi ya Elimu wakiwa na lishe duni ufaulu wao hautakuwa mzuri na tutasimamia kwa kutoa ushauri na huduma ya chakula Mashuleni.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Juni 16,2023.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa