• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MAADHIMISHO ya siku ya ualbino Kitaifa yafanyika Ruvuma

Posted on: June 13th, 2023

MAADHIMISHO ya Siku ya Kimataifa ya uelewa kuhusu Ualbino Kitaifa yamefanyika Mkoani Ruvuma.

Katika Maadhimisho hayo Mgeni rasmi alikuwa Waziri  wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu,Kazi,Vijana ,Ajira  na watu wenye ulemavu Joyce Ndalichako ,ambapo amewakilishwa na mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mkuu wa Wilaya ya Songea Wilman Ndile.

Ndile katika hotuba yake  amesema Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa Mikoa ambayo haijapata tukio la udhalilishaji kwa watu wenye ualbino kama mikoa  ya Kanda ya Ziwa.

“Hii kama mlivyoona katika Mkoa wa Ruvuma yangeweza kufanyika lakini kwaajili ya uongozi thabiti na wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kuwa waungwana na Mkoa umeendelea kuwa na amani na utulivu”.

Amesema Serikali imewapa kipaumbele wenye ulemavu ikiwa ni pamoja na maswala ya Elimu na uwezeshwaji wa kiuchumi,Afya, Ajira , mafunzo ya ufundi stadi pamoja na  nyenzo za kujimudu.

“Serikali ya awamu ya sita imeendelea na utekelezaji wa huduma ya watu wenye ulemavu Nchini imezingatia Sera,sheria,mikataba ya kikanda na Kimataifa”.

Kwa upande wake Kamishna msaidizi wa Jeshi la Polisi  Ralph Meela amesema  mara baada ya kuwepo kwa matukio mbalimbali kuanzia mwaka 2006 hadi 2017 matukioa ambayo yalitambuliwa na Jeshi la Polisi Nchini yalikuwa 73 ambayo yalitambuliwa  na kushirikisha imani za kishirikina.

Hata hivyo  Meela ameipongeza Serikali kwa Juhudi zinazosimamiwa na Rais akiwa ni amirijeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Nchini kwa kuhakikisha watu wenye ualbino wanakuwa salama.

“Mimi niseme tu kwa wenzetu wenye ualbino hali ya usala ni shwari tunawapa moyo na matumaini ulinzi umeimarishwa pande zote juhudi zilizofanywa na Serikalikwa kutoa Elimu”.

Hivyo amesema kuwa watu wenye ulemavu wa ngozi ni sawa kama wanadamu wengine ikiwa katika matukio 73 matukio 54 yalitokea kanda ya Ziwa kwaajili ya uchimbaji wa Madini na uvuvi  wa Samaki.

Amesema  Jeshi la Polisi wamechukua hatua ya kukamata waganga wapiga lamri chonganishi kwa kipindi cha mwaka 2014/2015 walifanya oparesheni ya kukamata  hao na matunguli yao wengine wamefungwa na wengine mpaka sasahivi wanatumikia vifungo vyao.

“Nitoe wito kwa watu  ambao wanaona watu wenye ualbino viungo vyao vinaweza kuongeza lolote katika maswala ya kiuchumi siyo kweli, wenzetu wenye ualbino waendelee kufanya shughuli zao tuna walinda na wahalifu waache mara moja tabia ya kutumia viungo vyao”.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Juni 13,2023. 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa