• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

KIONGOZI wa Mwenge wa Uhuru 2023 aweka jiwe la msingi katika mradi wa vijana wenye thamani ya shilingi milioni 44

Posted on: April 19th, 2023

 Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Abdalla Shaib Kaim ameweka jiwe la Msingi katika Kikundi cha vijana cha kufyatua tofali cha Madaba kwetu kilichopewa Mkopo wa asilimia 10 unaotokana na Mapato ya ndani.

Kiongozi huyo mara baada ya kuweka jiwe hilo la Msingi ameipongeza Halmashauri kwa kuunga Mkono Kauli mbiu ya utunzaji wa Mazingira pamoja na kuwawezesha vijana na makundi ya watu wenye mahitaji maalumu na kutekeleza maagizo kutoka Serikali kuu.

“Tumekagua mradi na nyaraka tumeona vigezo na ubora vimezingatiwa na mradi unauhalisia ikiwa ni pamoja na utunzaji wa mazingira mmefanya vizuri tuwapongeze vijana hawa”.

Kaim ametoa rai kwa vijana kutumia fursa pamoja na kubuni miradi ya maendeleo mbalimbali ikiwa kujiajili na kuacha  kujishughulisha na kazi ya wizi,ujambazi na madawa ya kulevya.

“Serikali inadhamira ya dhati fedha ipo nyingi inatolewa kwa kukopesha sambamba na fedha inayotolewa na  Halmashauri upo mfuko wa uwezeshaji kupitia mfuko wa Waziri Mkuu  tunakopesha mtu mmoja mmoja,kikundi mpaka Kampuni hadi kufikia milioni 50 vijana wenzangu walichokifanya ni fursa na uzalendo mkubwa”.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru ametoa rai kwa vijana wa kitanzania kuiga na kutumia fedha hizo kwa kujikwamua na kujipatia ajira.

Hata hivyo ameendelea kutoa rai kwa vijana wa kikundi hicho kurejesha marejesho kwa wakati ili na wengine waweze kupatiwa mikopo hiyo,pia amewaomba viongozi wa Halmashauri kuwapa kipaumbele cha tenda zinazojitokeza katika Halmashauri hiyo.

Katibu wa kikundi hicho Tumaini Wendalage akisoma taarifa kwa kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru Kitaifa 2023 amesema Halmashauri wamewakopesha kiasi cha shilingi milioni 44 ambazo zimewawezesha kujenga ofisi pamoja na ununuzi wa Mashine ya umeme yenye uwezo wa kufyatulia matofali 1000 kwa siku.

Hata hivyo wendalage ameeleza kikundi hicho kina wanakikundi 8 wakimwemo vijana wa kike 5 na vijana wa kiume 3 ,pia amesema kupitia kikundi hicho kitasaidia kutoa ajira kwa vijana wengine katika Halmashauri ya Madaba

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Halmshauri ya Wilaya ya Madaba

Aprili 19,2023.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa