• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

KAMATI ya kudumu ya Bunge ilivyotembelea eneo la uwekezaji wa Kilimo Ndolela

Posted on: March 15th, 2024

KAMATI ya kudumu ya Bunge Utawala Katiba na Sheria imetembelea eneo la uwekezaji  wa kilimo cha Mbegu shamba la Silver land Ndolela  lenye Hekta 5000  Jimbo la Madaba.

Akizungumza katika ziara hiyo Mwenyekiti wa kamati,  Mbunge wa Jimbo la Madaba Joseph Mhagama amesema Wabunge wamepata fursa ya kutembelea eneo la uwekezaji wa kilimo cha mbegu Jimbo la Madaba.

“Tumepata fursa ya kutembelea sekta ya viwanda lakini Waheshimiwa Wabunge hawakupata fursa ya kutembelea kwenye sekta ya kilimo,huwezi kuchukua changamoto ya viwanda kuleta kwenye kilimo itakuwa vizuri Kamati inapoenda kuandaa bajeti ijue changamoto ya sekta hii”.

 Mhagama amesema ziara yao katika eneo hilo imeleta fursa ya kujifunza ili waweze kushauri serikali  kuhusu sekta hii.

“Tunajua vikwazo  mbalimbali Wabunge wengi tunatoka kwenye familia ambazo wanalima lakini pengine hatujapata fursa ya kujifunza uwekezaji katika sekta ya kilimo kwa kiwango kikubwa”.

Hata hivyo Mhagama amesema uwekezaji huo utaimalika zaidi kama barabara ya kutoka Madaba na kuungana na Wilaya ya Ludewa itatengenezwa kwa kiwango cha Lami ikiwa kuna fursa ya uchimbaji wa chuma na wananchi wanaofanya kazi katika maeneo haya wanachukuliwa katika Kijiji cha Madaba na  Mavanga ambao ni Halmashauri ya Ludewa Mkoa wa Njombe.

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Machi 14,2024.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa