• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

HEKTA 40,000 kupandwa Miti ya biashara Ruvuma

Posted on: January 28th, 2021

MKOA wa Ruvuma umelenga kupanda miti ya biashara katika eneo lenye ukubwa wa hekta 40,000 hadi kufikia mwaka 2025.

Mshauri wa Maliasili na Utalii wa Mkoa wa Ruvuma Afrikanus Challe amesema  mradi huo unatekelezwa kwa miaka kumi kuanzia mwaka 2015,unatekelezwa kwa kupanda miti maeneo ya serikali kuu,serikali za mitaa,vyuo,shule na vijiji.

Challe ameitaja aina ya miti inayopandwa ni ile ambayo inafaa kwa ajili ya malighafi za viwanda vya mazao ya misitu ambayo ni misindano (pine),milingoti(Eucalyptus) na misaji(Teak).

‘Hadi kufikia mwaka 2020 jumla ya miti ya biashara iliyopandwa na wakala wa Huduma za misitu Tanzania(TFS) ni msitu wa hekta 4785,Halmashauri zilipanda miti hekta 425,vyuo na shule hekta 420 na watu binafsi hekta 23,964.

Amesema jumla ya mashamba yote ya miti yaliyopandwa katika kipindi hicho ni hekta 29,194 sawa na asilimia 56.1 ya lengo.

Kwa mujibu wa Mshauri huyo wa Maliasili na Utalii,Mkoa wa Ruvuma unalenga kuanzisha mashamba mapya mawili ya miti ya misaji katika Wilaya za Tunduru na Nyasa.

Kwa upande wake Mratibu wa kuendeleza Program ya mnyororo wa thamani wa mazao ya misitu(FORVAC) Mkoa wa Ruvuma Marcel Mtunda  amesema  wameandaa miche ya miti ya biashara aina ya misaji,pine na Eucalyptus ipatayo 4,000,000 ambayo itapandwa maeneo maalum yaliyotengwa na Mkoa yakiwemo Ifinga, Liuli, Liumbe, Upolo,Mpepo,kipiki na Kihangamahuka.

Amesema Mkoa unatekeleza mradi wa kuongeza thamani mazao ya misitu na nyuki kwa kushirikiana na FORVAC  na kwamba mradi unatekelezwa katika wilaya zote tano za Mkoa wa Ruvuma.

“Mradi huu utawezesha vijiji kutunza misitu ya hifadhi ya vijiji na kuwawezesha kupata faida kwenye misitu hiyo,hadi sasa wilaya ya Tunduru imeshapata mashine moja ya kuchana mbao ambayo imeanza kufanyakazi katika kijiji cha Sautimoja’’,alisema Mtunda.

Hata hivyo amesema Mkoa kwa kushirikiana na FORVAC imeomba mashine nyingine tatu ili zitumike katika wilaya za Namtumbo,Songea,Mbinga na Nyasa na kwamba mradi utasaidia kupunguza gharama za serikali kutekeleza miradi ya kimkakati ya kujenga shule,zahanati na madawati.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Januari 28,2020

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa