• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

HALMASHAURI ya Madaba yajiwekea mikakati ya kutatua changamoto za Lishe mwaka wa Fedha 2023/2024

Posted on: July 15th, 2023

HALMASHAURI ya Wilaya ya Madaba wamefanya Kikao cha utekelezaji wa afua za Lishe robo ya nne 2023.

Afisa Lishe wa Halmashauri hiyo John Mapunda amesema mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa  robo ya nne 2023 ikiwemo kufanya tathimini ya hali ya Lishe kwa Wanafunzi 135 wenye umri wa miaka 5-17 wa Shule ya Msingi Matetereka siku ya maadhimisho ya Siku ya  Mtoto wa Afrika Juni 16,2023.

Amesema watoto waliokuwa na uzito uliozidi  asilimia 2.9 na waliokuwa na hali nzuri ya Lishe ni asilimia 91.1 pamoja na waliokuwa na Lishe duni 6.1.

Mapunda amesema pia wamefanikiwa kufanya tathimini ya hali ya Lishe kwa watu wazima wenye umri wa mika 18 na kuendelea katika Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Aprili 19,2023  katika Halmashauri hiyo jumla ya watu 322 walifanyiwa tathimini, hali duni ya lishe ilikuwa asilimia 5,hali nzuri ya Lishe asilimia 66 na wenye hali ya Lishe iliyokithili asilimia 29, kutoa matone ya vitamini “A” kwa Watoto walio na umri wa miezi 6-59 wapatao 6691.

Hata hivyo Afisa Lishe amesema changamoto zilizojitokeza ikiwemo kutojengewa uwezo wa masuala ya Lishe kwa waratibu wa Lishe ngazi ya vituo vya huduma ya afya ambapo  kupelekea kuathiri utoaji wa huduma sahihi za Lishe.

Ukosefu wa iodine-RTK kupelekea kutopima madini joto kwenye chumvi ngazi ya Halmashauri .

Mapunda ameitaja mikakati ya kutatua changamoto hizo ikiwemo Halmashauri kutenga fedha kupitia mapato ya ndani kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ili kuwajengea uwezo waratibu wa vituo vya kutolea huduma za afya juu ya masuala ya Lishe,pamoja na kufanya maoteo ya mahitaji ya iodine RTK na kuwasilisha Wizara ya Afya.

Amesema kuendelea kufanya maadhimisho ya Siku ya Afya na Lishe ya Kijiji ilikuwezesha elimu ya Lishe kuwafikia jamii,Pamoja na kuimarisha utoaji wa Elimu kupitia wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii na watoa huduma ngazi ya kitu.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Julai,15,2023

 

 

 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa