• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

HALMASHAURI ya Madaba yaibuka nafasi ya Pili Kimkoa Matokeo ya Darasa la Saba

Posted on: January 18th, 2023

Halmashauri ya Wilaya ya Madaba imeibuka ushindi wa nafasi  ya pili Kimkoa Mtihani wa Darasa la Saba kwa miaka miwili mfululizo kwa asilimia 80.89.

Hayo amesema Mkuu wa Idara ya Elimu Msingi Saada Chwaya ofisini kwake kuwa 2021 waliibuka kwa ushindi wa nafasi ya pili kimkoa na 2022.

“Halmashauri ya Madaba tumekuwa nafasi ya pili Kimkoa kwa miaka miwili mfululizo kwa asilimia 80.89 “.

Chwaya amzitaja Shule tano bora katika Halmashauri hiyo mwaka 2022 zilizoongoza kwa  kufanya vizuri ST.Getrude wastani wa 205.27,Mkwera wastani wa 189.46,Njegea wastani wa 170.61,Kifaguro wastani wa 167.73 pamoja na Ifugwa wastani wa 164.78.

Hata hivyo ameyataja mambo yaliyosababisha kupaata ushindi wa nafasi ya pili ikiwa nipamoja na kufanya ufuatiliaji wa mara kwa mara mashuleni,kufanya mitihani ya kutosha iliyozingatia mfumo mpya wa utunzi.

Pia kuwaandaa wanafunzi kujiamini kuanza kujitegemea wao wenyewe katika mitihani,kuwepo kwa msisitizo wa kila Shule kuwa na kamati hai za uthibiti Ubora wa ndani ya Shule ambao utaratibu wa ufundishaji na ujifunzaji,utoaji wa mazoezi, ukamilishaji wa mada,utunzi wa mtihani na ufanyaji wa masahihisho ya kina wa mazoezi ya mitihani.

Chwaya ameeleza changamoto zilizojitokeza katika ngazi ya Shule kutokuwa na walimu wa kutosha kutokana na Walimu wengi kustaafu na ongezeko la wanafunzi kila mwaka.

Amesema kukosekana kwa walimu mahiri wa baadhi ya masomo,baadhi ya Shule kutoelewa vyema mkakati wa kuongeza ufaulu kwa kufuta daraja D na E,baadhi ya Walimu kutokamilisha mada zao kwa wakati hivyo kusababisha baadhi ya mada kuto fundishwa kabisa.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka:Kitengo cha Mawasiliano Serikalini ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Madaba

Januari 18,2023.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa