• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

HALMASHAURI ya Madaba Mkoani Ruvuma yaongoza ufaulu miaka 3 Mfululizo

Posted on: April 12th, 2021

HALMASHAURI ya Wilaya ya Madaba imefanya tathimini ya maendeleo ya  Elimu na kufikia kufanya vizuri miaka mitatu mfululizo mwaka 2018-2020.

Akifungua kikao hicho Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololeti Mgema amesema Mkutano kama huu hufanyika kila mwaka na kujiwekea mikakati ya kufanikiwa zaidi katika sekta ya Elimu.

“Tunapozungumzia tathimini ya Elimu tunawagusa moja kwa moja walimu,maswala mengine tunapoona tumekwama  moja kwa moja hili swala linakuwa la walimu wametukwamisha na tukifanikiwa tunasahau kusema tumefanikiwa kwa sababu ya walimu  tunaomba mtuvumilie”.

Mkuu wa Wilaya amewaomba walimu kuwa huru kuzungumza changamoto zao mambo yaliyopelekea kufanya vizuri na yaliyokwamisha kutofa fanyika vizuri katika sekta ya Elimu.

Mgema ametoa rai kwa Madiwani wa Halmashauri hiyo kutoa changamoto zinazozikabili shule ambazo zipo kwenye kata zao ili ziwekewe mikakati ya kuzitatua hatimaye kufanya vizuri zaidi.

“Tunatambua uwepo wa wadau wengine kama mchango wa bank yaNMB katika Halmashauri ya Madaba wametuchangia kwa kiasi kikubwa katika sekta ya Elimu,pia TFS nao wametuchangia kwa kiasi kikubwa sana kama mabati,saruji tunaomba muendelee kusukuma gurudumu la Elimu katika halmashauri yetu ya Mdaba’’.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Shafi Kassim Mpenda katika kikao hicho amesema mbinu zinazotumika katika  kuhakikisha wanafunzi wanadhulia masomo yao vizuri na kufanya zizuri darasani  wameweka utaratibu wa kuwatumia watendaji,waratibu wa elimu kata katika ufuatiliaji.

Hata hivyo Mpenda amesema pia wameweka mkakati wakufanya mitihani ya muhula na nusu muhula na pale tu wanapofungua shule wanafanya mitihani iliyopelekea Halmashauri hiyo kufanya vizuri.

“ Tumeimarisha utawala bora shuleni tumekuwa na vikao vya mara kwa mara na walimu wakuu bodi za shule na vikao vya wazazi na kazi hiyo ni endelevu hata kwa walimu wanaokiuka tunawasikiliza kabla ya kuwachukulia hatua, na kuhakikisha walimu wanafanya kazi katika mazingira rafiki japo siyo rafiki kwa asilimia mia moja”.

Kwa upande wake makamu mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Orap Pili amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kwa usimamizi  na walimu wote kwa kazi nzuri wanayofanya na kufikia kuongoza kwa miaka mitatu mfululizo na kupata heshima kubwa katika Halmashauri ya Madaba.

Aidha Makamu Mwenyekiti ameendelea kuwaomba walimu wa Halmashauri hiyo kuwa wavumilimu kutokana na changamoto zinazojitokeza katika mazingira magumu,kwa niaba ya Madiwani amewaahidi walimu kushirikiana  katika maeneo ya kazi katika kata na kufuatilia maazimia yaliyowekwa.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Afisa habari Halmashauri ya Madaba

April 12,2021.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa