• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika

HALMASHAURI ya Madaba kuanza uchimbaji wa Mkaa ya Mawe Machi 2023

Posted on: January 23rd, 2023

Kampuni mbili zinatarajia kuanza uchimbaji wa Makaa ya Mawe katika Halmashauri ya Madaba katika Kata ya Mtiyangimbole na Gumnbiro ifikapo Machi 2023.

Hayo ameyasema Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Sajidu Idrisa Mohamed katika kikao cha Baraza la Madiwadi cha robo ya pili ya  mwaka 2022/2023.

“Tumeshapata kampuni mbili tayari zimeonyesha nia na zimetamburishwa kwa Katibu Tawala wa Mkoa na Wilaya ambazo zinatarajia kuanza uchimbaji wa makaa ya mawe Machi katika Kata ya Mtiyangi Mbole”.

Hata hivyo Mkurugenzi amewaomba  Waheshimiwa Madiwani wanaotoka katika Kata ya Mtiyangimbole na Ngumbiro kuwapa ushirikiano wataalamu wa uchimbaji wa makaa ya mawe.

Amesema katika uchimbaji wa Makaa ya Mawe kuna faida nyingi zitapatikana katika  Halmashauri ya Madaba kwa kuongeza uwigo wa mapato ikiwa ni adhima ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Wapo tayari kuhakikisha sehemu ambazo watapita na Makaa ya Mawe barabara watatengeneza wenyewe”.

Mkurugenzi amesema wananchi wa maeneo hayo ni fursa kwa kujenga Hotel pamoja na huduma zingine ikiwa ni pamoja na Halmashauri kujipatia fedha na kukua kiuchumi

“Hizo ni kampuni mbili lakini zipo nyingi ambazo zitaendelea kujitokeza  kuwekeza katika Halmashauri ya Madaba hizo ni fursa kwetu kuhakikisha tunatangaza rasilimali  zilizopo katika Halmashauri ya Madaba ambapo tulikuwa tunategemea kilimo pekee”.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo amempongeza Mkurungenzi na wataalam kwa kufanya uchunguzi wa uchimbaji wa Makaa ya Mawe katika Kata ya Mtiyangimbole na  Gumbiro amesema uchimbaji huo utasaidia kuongeza uchumi katika Halmashauri ikiwa mwanzo walitegemea mapato kupitia kilimo cha chakula.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Teofanes Mlelwa katika Baraza hilo amewapongeza wataalamu wote kwa utendaji kazi na hasa katika  usimamiaji wa miradi ya maendeleo katika Kata zote.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Madaba

Januari 23,2023.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • TANGAZO LA AJIRA ZA SENSA May 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 10, 2021
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • WANAFUNZI wa shule ya Sekondari Joseph Kizito Mhagama wapanda miti 800

    January 29, 2023
  • JUMUIYA ya wazazi Wilaya ya Songea waadhimisha miaka 46 ya CCM kwa kupanda miti Madaba

    January 29, 2023
  • Heri ya siku ya kuzaliwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    January 27, 2023
  • RUVUMA waadhimisha kuzaliwa kwa Dkt Samia kwa kupanda miti

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

MADABA KUANZA KUCHIMBA MAKAA YA MAWE
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 10

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: info@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa