• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

DC Songea:watendaji iwe mwisho kuzungumzia wanafunzi kuripoti shuleni Februari 27,2024

Posted on: February 7th, 2024

MKUU wa Wilaya ya Songea Kapenjama Ndile amewaagiza watendaji kuhakikisha ifikapo Februari 27,2024 kufuta suala la kuzungumzia wanafunzi waliopangiwa kuripoti Shuleni Januari 2024 linafika tamati.

Hayo amezungumza katika kikao kazi cha Wakuu wa Shule,Maafisa Elimu,Watendaji Kata na Vijiji kilichofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari  Madaba day.

Aidha Mkuu wa Wilaya amewaagiza Wakuu wa shule kusimamia Kilimo cha Maharage Lishe aina ya Jesca na mahindi lishe yaliyotolewa kwaajili ya kuzalisha Mbegu mashuleni.

“Niwaombe mbegu mlizopewa hakikisheni mnazalisha ili wapate na shule zingine na tuweze kutokomeza udumavu kwa watoto”.

Katika kikao hicho Ndile amewaagiza walimu hao kuhakikisha wanalima bustani za mbogamboga na matunda ili kuhakikisha wanafunzi  wanakula chakula bora na kuwa na afya njema ili waweze kufanya vizuri katika masomo yao.

Hata hivyo Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Madaba Maternus Ndumbaro amesema wanafunzi waliopangiwa kujiunga kidato cha kwanza Januari 2024 walikuwa 1254 walioripoti  hadi kufikia sasa 1048 wasichana 506 na wavulana 542 sawa na asilimia 83.55.

Upande wa Elimu Msingi darasa la awali wameripoti wanafunzi 1797 sawa na asilimia 100.11 na darasa la kwanza hadi kufikia sasa wameripoti 1749 sawa na asilimia 99.94.

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Februari 7,2024.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa