• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

DC SONGEA:Mkurugenzi simamia Fedha za miradi kwa Uaminifu na uadilifu

Posted on: August 22nd, 2021

MKUU wa Wilaya ya Songea Mheshimiwa Pololeti Mgema ametoa maelekezo  kwa Mkurugenzi wa Halmashauri  ya Madaba kusimamia fedha za miradi kwa uaminifu na uadilifu, ikiwemo Madarasa ambayo ameelekeza kuwa  yakamilike kwa wakati.

Hayo ameyasema katika Kikao cha Baraza la Madiwani kilichopokea taarifa ya utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya halmashauri yaliyotekelezwa katika  robo ya nne ya mwaka wa fedha 2020/2021. Kikao hicho kilichofanyika tarehe 21/08/2021 katika Ukumbi wa Halmashauri.

Mhe. Pololeti Mgemaalisema kuwa, fedha zinazoletwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya wananchi zisimamiwe  kwa uaminifu na kwa uadilifu ili Halmashauri ya Madaba iendelee kutekeleza miradi yenye viwango vinayolingana na fedha zinazoletwa kutoka Serikalini.

Mh. Pololeti Mgema amesema, fedha zilizotolewa kwa ajili ya Madarasa shilingi milioni kumi na mbili na laki tano (12,500,000/=) zinaweza kukamilisha majengo ambayo yameanzishwa kwa nguvu za wananchi. Aidha amesema kuwa, madarasa yaliyoletewa  shilingi milioni 20 (kwa kila darasa) zitumike kwa ajili ya ujenzi wa madarasa mapya kuanzia msingi hadi kumaliza bila kuwachangisha wananchi.

Alimuagiza Mkurugenzi akisema,“Fuatilia mahali ambapo tumejenga madarasa ambapo wananchi waliambiwa watoe tofali na nguvu zingine. Kile ambacho walichangia kibadilishwe kuwa gharama na iwe sehemu ya kuokoa fedha kwenye mradi huo, tuokoe fedha kwa sababu wananchi walichangia”alisisitiza.

Hata hivyo amelaani kitendo cha kusimamisha kazi ya ujenzi wa madarasa ya shule ya msingi katika kijiji cha likalangilo kwa sababu  wananchi hawajaleta tofali za kutosha na amemwagiza Mkurugenzi kufuatilia swala hilo.

“Wananchi wanajitoa katika shughuli za maendeleo na Waheshimiwa Madiwani wanajitoa, huo ni msaada wako maana umekuja kwenye Halmashauri ambayo Madiwani ni wamoja hakuna migogoro ya wenyewe kwa wenyewe wala  migogoro ya Madiwani na watumishi, uwaweke watumishi wafanye kazi kwa bidii ili serikali isipate hasara ya kulipa mtumishi mvivu”.amesisitiza Mgema.

Amesema Serikali kwasasa inaleta fedha ya miradi kwa kiwango kikubwa ikiwemo milioni 500 zilizoletwa kwa kila Halmashauri lakini Madaba imetengewa bilioni moja kwa ajiji ya matengenezo ya barabara. Fedha hizi zisimamiwe vizuri.

Mh. Mgema ametoa maelelekezo katika Baraza hilo kuwahamasisha wananchi kujiunga na CHF iliyoboreshwa ili kupata huduma bora ya afya kwa shilingi elfu thelatini kwa mwaka, na kumwagiza Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo kuhakikisha kuwa, kituo cha Afya Mtyangimbole kuanza kufanya kazi na huduma zote zitolewe kwa sababu kituo hicho kimekwisha kukamilika.

Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bw. Sajidu Idrissa Mohamed katika Baraza hilo ikiwa ni kikao chake cha kwanza  amemshukuru Rais kwa kumuona na kumleta Madaba, ameomba ushirikiano kwa Wataalamu ili kuhakikisha Halmashauri  inasonga mbele katika Nyanja zote.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Teophanesi Mlelwa  wakati akifunga kikao hicho ameahidi kutoa ushirikiano kwa Mkurugenzi mpya katika utendaji wa kazi na amewaomba watumishi na Waheshimiwa Madiwani kumpa ushirikiano  ili kuhakikisha Halmashauri hiyo inaendelea kufanya vizuri.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Afisa Habari Halmashauri ya Mdaba

Agosti 22,2021

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa