• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

DC Songea azindua upandaji wa miti Madaba

Posted on: January 1st, 2023

MKUU wa Wilaya ya Songea Pololeth Mgema amezindua upandaji wa Miti na kugawa kwa wananchi katika Kijiji cha Lilondo Kata ya Wino Halmashauri ya Madaba.

Akizungumza katika uzinduzi huo Mgema ameelezea umuhimu wa uwepo wa miti katika mazingira inasaidia katika kuleta hewa safi oksijeni na kunyonya hewa ya kabonidayoksaidi  ambayo ni hewa chafu anayotoa mwanadamu.

“Sisi na Miti ni marafiki mmoja akikosekana mwingine hawezi kuishi atakufa kwasababu ya hewa tunayobadilishana “.

Hata hivyo Mkuu wa Wilaya amesema Dunia ipo katika janga la ukame ambalo linasababishwa na shughuli za kibinadamu ikiwemo kilimo,ufugaji ukataji wa kuni,mkaa na mbao.

Amesema uwiano wa ukataji miti na upandaji wa miti kila mwaka haulingani kwa sababu miti inayopandwa ni michache kutokana na ukataji miti na inayopandwa ni michache.

“Serikali zote Duniani kila mwaka inakutana kwenye mkutano wa mazingira kujadili namna ya kuikarabati dunia iweze kuwa mahali pakuishi”.

Kwaupande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Sajidu Idrisa Mohamed amewapongeza wananchi hao kwa kujitokeza katika kupanda miti siku ya Januri 1 ikiwa ni siku ya sikukuu

Amesema zoezi hilo la upandaji wa miti limeanza tangia Desemba 31 katika Hospitali ya Wilaya na miti iliyopandwa ni 500  na eneo la Shule ya Lilondo 500 jumla imepandwa 1000.

Mohamed ametoa wito kwa wananchi kufika katika ofisi ya Halmashauri na kuchukua miche ya kupanda katika maeneo yao na vyanzo vya maji  na kuhakikisha miti hiyo inatunzwa.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Madaba

Januari 1,2022.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa