• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

BARAZA la Madiwani Madaba lapitisha mpango wa bajeti 2023/2024 ya matengenezo ya barabara

Posted on: February 13th, 2023

Katika mwaka wa fedha 2023/2024 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba imepanga kutumia zaidi  ya shilingi bilioni 2 katika matengenezo ya Barabara.

Hayo ameyasema kaimu Meneja wa Wakala wa barabara vijijini (TARURA)

Godfrey Mngale katika kikao cha Baraza la Madiwani kilicho fanyika katika ukumbi wa Halmashauri.

Hata hivyo amesema Halmashauri imepanga kutumia kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 613 kwa matengenezo ya mtandao wake wa barabara,matengenezo ya kawaida ikiwa fedha zilizotengwa kiasi cha shilingi milioni 12 ambazo zinatarajia kufanya matengenezo yenye jumla ya kilomita 3.0

Amesema sema matengenezo sehemu kolofi fedha zilizotengwa kiasi cha shilingi milioni 186 ambazo zinatarajia kufanya matengenezo ya kilo mita 2.2 pamoja na matengenezo maalumu kiasi cha  zaidi ya shilingi milioni 415 ambazo zinatarajia kufanya matengenezo yenye jumla ya kilomita 22.79.

Mngale amesema milioni 500 zimetengwa kwaajili ya barabara za changarawe kilomita 44.7,bilioni moja ambayo inatarajia kujenga barabara ya Lami yenye kilomita 1.5 pamoja na daraja na matengenezo ya barabara kilomita 3.5.

Makamu mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Olaph Pili amempongeza Mbunge wa jimbo la Madaba kwa kuhakikisha bajeti  ya matengezo ya  Barabara inapatikana.

Pia Pili amewapongeza wataalamu wa TARURA pamoja na watumishi wote wa Halmashauri inayoongozwa na Mkurugenzi mtendaji Sajidu Idrisa Mohamed kwa utendaji kazi na kuhakikisha Halmashauri ya Madaba inafunguka kwa maendeleo.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Madaba

Februari 13,2023.

 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa