• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

AGOSTI 2022 Wananchi mjitokeze kuhesabiwa

Posted on: March 9th, 2022

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amehamasisha wananchi ifikapo Agasti kujitokeza kuhesabiwa.

Hayo amesema katika kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani,kimkoa imefanyika katika Halmashauri ya Mdaba Wilaya ya Songea na ameeleza faida ya Sensa ya watu na makazi.

Amesema zoezi hilo litawezesha Taifa kupanga mipango ya Maendeleo ya mda mfupi na mrefu kwa mstakabali ya maisha ya wananchi zoezi hilo linaendelea na uwekaji wa anwani za makazi na postikodi ili tuwe na uhakika wa kufanikisha sense ya mwaka huu.

“ Niwakumbushe kuwa mwa huu tunafanya sensa ya watu na makazi Hivyo niwahimiza wananchi wote kujitokeza kuhesabiwa “.

Ibuge katika halfu ya shelehe hizo amesema Serikali ya awamu ya sita imekuwa mstari wa mbele kuwawezesha wanawake kwa njia mbalimbali ikiwemo kupokea fedha kupitia mpango wa Maendeleo kwa Taifa na mapambano Dhidi ya Uviko 19 kwenye sekta ya Afya.

Amesema fedha hizo ni kwaajili ya kujenge majengo matatu ya dharura,Jengo la wagonjwa mahututi moja kwa lengo la kuhakikisha wanawake wajawazito na watoto wadogo chini ya umri wa miaka mitano wanapata huduma nzuri.

Hata hivyo Ibuge amesema katika eneo la kuendelea kujikinga na VVU-UKIMWI janga bado lipo ni jukumu la wazazi na walezi kujilinda na kuelimisha jamii na kujihadhali na janga hili.

Ibuge ameipongeza Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia kwa kusimamia kwa ukaribu wa utoaji wa mikopo isiyo na riba kwa wanawake inayotokana kwa asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri.

Akisoma Risala mwakilishi wa Wanawake  Mariam Juma amesema Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa Mikoa iliyoathirika na Janga la UKIMWI hivyo wamejiwekea mikakati ya kutoa elimu,kupima afya kwa hiari,kutoa huduma kwa watoto yatima pamoja na kukemea mila na desturi zinazochochea maambukizi.

Ikiwemo kurithi wajane,ngoma za usiku,ulevi uliokithiri,kuendekeza ngono zembe na kutoa msisitizo wa wananchi kubadili tabia zao.

Juma ameeleza changamoto wanazokabiliwa ikiwemo fedha za mikopo zinazotolewa hazitoshelezi kuwapatia vikundi vyote kulingana na uhitaji,Vikundi kutorejesha mikopo kwa wakati pamoja na uelewa mdogo kwa jamii kuhusu elimu ya usawa na jinsia.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Machi 9,2022.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa