• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

SIKU YA WAZEE DUNIANI YAFANA MKOANI RUVUMA

Posted on: October 1st, 2025

Maadhimisho ya kilele cha Siku ya Kimataifa ya Wazee Duniani mwaka 2025 yamefanyika leo, Oktoba 1, 2025, katika Ukumbi wa Songea Club, Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma, yakiambatana na kaulimbiu isemayo “Wazee Tushiriki Uchaguzi kwa Ustawi wa Jamii Yetu.”

Sherehe hizo zimekusanya mamia ya wazee kutoka mikoa mbalimbali nchini, zikiwa na lengo la kuhamasisha ushiriki wao katika mchakato wa kidemokrasia pamoja na kuenzi mchango wao katika historia na maendeleo ya taifa.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, Bi. Marry Makondo, alisema wazee ni hazina ya hekima na dira ya taifa, hivyo jamii ina wajibu wa kuwatunza na kuwathamini.

Kwa upande wake, Mratibu wa Huduma kwa Wazee kutoka TAMISEMI, Bw. Haroun Yunus Haroun, alieleza kuwa serikali imefanikiwa kuwatambua wazee kwa kuwapatia vitambulisho pamoja na bima ya afya. Aidha, halmashauri 184 nchini zimeanzisha jumla ya madirisha 4,094 ya huduma kwa wazee, hatua inayoongeza upatikanaji wa huduma rafiki.

Naye, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la Taifa, Bw. David Sendo, alisisitiza kuwa mshikamano na amani ya taifa ni matunda ya hekima ya wazee waliotangulia, hivyo vijana wanapaswa kujifunza na kuthamini mafunzo yao.

Akizungumza kwa niaba ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Naibu Katibu Mkuu, Wakili Amon Mpanju, alihimiza jamii kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya wazee huku akisisitiza usawa na heshima kwa makundi yote ya kijamii.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Brigedia Jenerali Ahmed Abbas, aliwahimiza wananchi kutumia kaulimbiu ya mwaka huu kama mwongozo wa kuichagua serikali ambayo inajali, sikivu na kutambua changamoto za wazee. Alisisitiza kuwa wazee wanastahili heshima, ushirikishwaji katika masuala ya kijamii na kitaifa, ikiwemo upatikanaji wa huduma muhimu.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • DED MADABA APIGA KURA KATIKA KITUO CHA SHULE YA MSINGI KIFAGURO

    October 29, 2025
  • MAFUNZO YA WASIMAMIZI WA VITUO NA WASIMAMIZI WASAIDI YAFUNGWA RASMI, MSISITIZO WAWEKWA KWENYE UZALENDO NA UADILIFU.

    October 27, 2025
  • WASIMAMIZI WAKUU WA VITUO VYA UCHAGUZI NA WASIMAMIZI WASAIDIZI WAPIGWA MSASA MADABA

    October 26, 2025
  • MKUTANO MKUU WA 32 WA WINO SACCOS WAFANA MADABA

    October 25, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa