• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

RC:Ibuge aziagiza Halmashauri kudhibiti vitendo vya utoroshwaji wa mazao

Posted on: May 13th, 2022

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amezitaka Halmashauri zihakikishe zinatoa elimu kuhusu mifumo ya masoko kwa wakulima na wadau wengine

Ameyasema hayo katika mkutano wa wadau wa mfumo wa Stakabadhi Ghalani uliofanyika katika ukumbi wa manispaa ya Songea

RC Ibuge amesema Halmashauri zihakikishe zinaweka usimamizi madhubuti wa vyama vya ushirika vya msingi na shughuli zote zinazohusu mifumo ya masoko hasa Stakabadhi Ghala.

“Wafanya biashara na wanunuzi wa mazao na vyama vikuu vya ushirika TAMCU na SONAMCU hakikisheni mnafanya malipo ya wakulima kwa wakati ili kufanya waupende mfumo huu vilevile muda wa kutekelezwa malipo uwe sehemu ya masharti ya ununuzi ”, amesema RC Ibuge.

Hata hivyo amesema uwekwe ukomo wa kiasi cha mazao yanayoweza kuuzwa nje ya mfumo wa Stakabadhi za Ghala kwa kuangalia nini kifanyike kuhusu wakulima wauze mazao machache wanayotaka kuuza na mengine kujikimu au kuhifadhi nyumbani.

Pia Halmashauri za Mkoa wa Ruvuma zihakikishe zinaandaa mapema mipango na mikakati endelevu ya usimamizi wa zoezi la uzalishaji, ukusanyaji wa mazao na mfumo mzima wa masoko ya mazao hayo ili kumsaidia mkulima kupata kipato chake  

Aidha, ametoa angalizo kwa wamiliki na wafanyabiashara wanaojishughulisha na kuhifadhi mazao kwenye maghala kuzingatia taratibu zilizowekwa katika uhifadhi wa mazao hayo watakaokiuka watachukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kufungiwa maghala yao.

Imeandaliwa na Bahati Nyoni na Jackson Mbano

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

13 Mei 2022.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa