• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MUFTI MKUU WA TANZANIA AWASILI MKOANI RUVUMA

Posted on: October 10th, 2025
Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Dr. Abubakary Zuberi bin Zuberi, amewasili mkoani Ruvuma kwa ziara ya kidini yenye lengo la kuimarisha ustawi wa jamii ya Kiislamu na kuhimiza mshikamano miongoni mwa waumini. Ziara hii ni sehemu ya juhudi za Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) katika kusogeza huduma na uongozi wa kiroho karibu na ngazi za chini.

Mapokezi ya Mufti Mkuu  katika Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, yakihudhuriwa na viongozi wa dini, serikali, na mamia ya waumini waliokusanyika kumpokea kwa shangwe na heshima. Sheikh wa Mkoa wa Ruvuma, Ramadhani Mwakilima, aliongoza mapokezi hayo na kueleza kuwa ujio wa Mufti Mkuu unaongeza ari kwa viongozi wa dini na waumini katika kushiriki shughuli za maendeleo na uimarishaji wa imani.

 Akitoa salamu zake, Sheikh Mwakilima alieleza kuwa ziara hiyo imekuja wakati muafaka, kwani inawapa waumini nafasi ya kupata maelekezo ya moja kwa moja kutoka kwa uongozi wa kitaifa wa BAKWATA, sambamba na kushirikiana katika kufanikisha miradi ya kijamii inayotekelezwa na taasisi hiyo. Aliongeza kuwa ni fursa ya kuimarisha mshikamano wa kidini na kijamii.

Mufti Mkuu, aliwashukuru wananchi wa Ruvuma kwa mapokezi ya upendo na mshikamano, akisisitiza kuwa umoja wa Waislamu ni chachu ya maendeleo ya kitaifa. Alihimiza viongozi wa dini kuendelea kuwa daraja la maelewano, huku akisisitiza jukumu la waumini kushiriki katika kulinda maadili, amani na ustawi wa jamii.

Akiwa mkoani Ruvuma, Mufti Mkuu atazuru wilaya za Songea, Namtumbo, Tunduru na Nyasa, ambako atakutana na viongozi wa dini, waumini na watendaji wa serikali. Aidha, atakagua na kuzindua miradi mbalimbali ya Kiislamu kama misikiti, shule, na vituo vya malezi ya watoto wa Kiislamu (madrasah), ikiwa ni ishara ya kuunga mkono maendeleo ya elimu na huduma za kijamii.

Ziara hii ni sehemu ya mpango mpana wa BAKWATA wa kujenga uhusiano thabiti kati ya makao makuu na viongozi wa mikoa, pamoja na kuhakikisha taasisi za Kiislamu zinatoa mchango chanya katika maendeleo ya taifa. Mufti Mkuu anatarajiwa kuhitimisha ziara yake kwa kutoa hotuba kwa viongozi wa dini na waumini kuhusu nafasi ya Waislamu katika kulinda amani na kulea kizazi chenye maadili bora

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • DED MADABA APIGA KURA KATIKA KITUO CHA SHULE YA MSINGI KIFAGURO

    October 29, 2025
  • MAFUNZO YA WASIMAMIZI WA VITUO NA WASIMAMIZI WASAIDI YAFUNGWA RASMI, MSISITIZO WAWEKWA KWENYE UZALENDO NA UADILIFU.

    October 27, 2025
  • WASIMAMIZI WAKUU WA VITUO VYA UCHAGUZI NA WASIMAMIZI WASAIDIZI WAPIGWA MSASA MADABA

    October 26, 2025
  • MKUTANO MKUU WA 32 WA WINO SACCOS WAFANA MADABA

    October 25, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa