• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MAADIMISHO ya wanawake duniani 2021 yalivyolenga usawa katika uongozi

Posted on: March 9th, 2021

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amehitimisha maadhimisho ya kilele ya siku ya wanawake Duniani  Mkoani Ruvuma.

Maadhimisho hayo yamefanyika kakatika kijiji cha Kalanje katika viwanja vya Baraaza la Idd ,Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma na kauli mbiu ikiwa Wanawake katika uongozi chachu ya kufikia dunia yenye usawa.

“Siku ya leo ni muhimu sana kwa Dunia nzima inaanzimisha siku ya wanawake,ambalo ni tukio muhumu katika jamii yetu kuweza kufahamu umuhimu na nafasi kubwa waliyonayo wanawake katika jamii yetu na katika uongozi wanchi katika kutoa mchango mkubwa wa malezi ya watoto”.

Mndeme amesema wanawake ni nguzo kubwa katika nchi yetu ndio wanaotoa dira na mwelekeo wa maendeleo katika ngazi zote za kifamilia hadi uongozi wa juu ya nchi.

Hata hivyo amesema serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua na kuthamini mchango unaotolewa na wanawake katika Taifa na kwakuliona hili iliamua kutoa mikopo kwa kuzitaka Halmashauri zote kutenga asilimia 4 ya mapato yake ya ndani ili kuhakikisha wanawake wanawezeshwa.

Amesema Mkoa wa Ruvuma Halmashauri zote kwa kipindi cha Julai 2020 hadi Februari 2021 zimetoa mikopo yenye thamani ya shilingi 444,167,441.82 kwa vikundi 603 vya wanawake,vikundi 221 vijana vikundi 203 watu wenye ulemavu watu wenye ulemavu vikundi 179.

“Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatekeleza kauli mbiu hii ya Wanawake katika uongozi chachu kufikia dunia yenye usawa hivyo kwa vitendo tunaona wakuu wa Mikoa/Mawaziri,wakuu wa Wilaya,Wakurugenzi na wakuu wa Idara ambao ni wanawake ni jukumu letu kuwapa wanawake nafasi ya uongozi”.

Afisa maendeleo ya Jamii wa Mkoa wa Ruvuma Zawadi Nyoni akitoa historia fupi ya siku ya wanawake duniani amesema ilianzishwa mwaka 1900 kufuatia maandamano ya wanawake wafanyakazi wa sekta ya viwanda nchini Marekani kupinga mazingira duni ya kazi.

Nyoni amesema walipinga wakilalamikia ukosefu wa huduma za kijamii na kuwepo kwa vitendo vya unyanyasaji katika ajira ikiwemo wanawake kulipwa mshahara mdogo kwa kazi sawa ukilinganisha na wanaume.

Amesema wanawake wa Mkoa wa Ruvuma wako mstari wa mbele katika Nyanja za kuleta maendeleo endelevu kwa Jamii ikiwemo kushiriki na kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Pia amesema wanawake wamekuwa mstari wa mbele kulaani vitendo vya kikatili dhidi ya wanawake na watoto hususani wa kike,kupinga matumizi ya madawa ya kulevya,na kupambana na janga la UKIMWI na magonjwa ya mlipuko kwa kutumia Elimu kwa jamii kwa njia ya sanaa.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Afisa habari Halmashauri ya Madaba

Machi 9,2021

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa