• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

KAIJAGE alivyosikiliza Kero za Watumishi Halmashauri ya Madaba

Posted on: November 16th, 2023

MBUNGE Viti maalumu anyewakilisha Watumishi Tanzania Ofisi ya Rais  Utumishi na Utawala bora  Alice Kaijage ametembelea Halmashauri ya Wilaya ya Madaba na kusikiliza kero na changamoto za watumishi.

Akizungumza katika kikao hicho kabla  ya kuwasikiliza watumishi hao Kaijage amewapongeza kwa kazi kubwa wanazofanya bila kujali changamoto nyingi wanazo kabiliana nazo katika utendaji kazi.

“Ningeweza kwenda kinondoni lakini nikaona nije Nyanda za juu kusini ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Madaba niwaone na niwasikilize ili nikawasemee”.

Hata hivyo Kaijange mara baada ya kuwasikiliza watumishi hao amesema changamoto zote walizozitoa atazifanyia kazi ili kuhakikisha watumishi wanafanya kazi katika mazingira rafiki.

“Bajeti iliyopita kwa miaka mitatu eneo la utumishi halikuachwa na Serikali imeweza kubadilisha miundo na Kada ya watumishi 30,245 na imehuishwa na kusainiwa na kuanzakufanya kazi  ilikuwa ni kilio cha miaka mingi”.

Kaijage  amesema bajeti ya miaka mitatu watumishi zaidi ya laki nne wamepandishwa madaraja na kugharimu zaidi ya Shilingi Tilioni moja ikiwa upande wa malimbikizo ya mishahara Rais amegusa kwa miaka mitatu na ajira mpya zaidi ya laki moja na ajira elfu 21 Serikali za Mitaa.

“Nasema hayo kwasababu  niko kazini  Rais Samia ni msikivu amefanya kazi  kubwa na anania njema na watumishi”.

Hata hivyo amesema Serikali ya awamu ya sita inagusa kila idara ikiwemo miradi ya Afya na Elimu,na watumishi ikiwa kwa muda wa miaka  mitatu ameshusha fedha nyingi katika Halmashauri zote Tanzania hivyo ametoa rai kuendelea kumuunga mkono  Rais kwa kufanya kazi kwa bidii.

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

Novemba 15,2023.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa