• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

HALMASHAURI YA MADABA YAPOKEA MEZA NA VITI 40 KUTOKA BENKI YA CRDB

Posted on: October 9th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Madaba mkoani Ruvuma imepokea jumla ya meza na viti 40 kwa ajili ya Shule ya Sekondari Mtyangimbole kutoka Benki ya CRDB Kanda ya Kusini, ikiwa ni sehemu ya juhudi za benki hiyo kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuboresha sekta ya elimu nchini.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, Wakili Sajidu Idrisa Mohamed, ameishukuru Benki ya CRDB kwa mchango huo muhimu na kuipongeza kwa kujali juhudi za Serikali katika kuhakikisha elimu bora inapatikana kwa wanafunzi wote nchini.

Aidha Mkurugenzi, amewataka wanafunzi wa shule hiyo kutunza viti na meza walizokabidhiwa, huku akimwagiza Afisa Elimu Sekondari kuhakikisha hatua kali zinachukuliwa dhidi ya wanafunzi watakaoharibu mali za shule. 

Pia, amesisitiza kuwa ujenzi wa Shule ya Sekondari Mtyangimbole yenye thamani ya shilingi milioni 560 ni uthibitisho wa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha miundombinu ya elimu na kuwaondolea wanafunzi adha ya kutembea umbali mrefu kufuata masomo.

Kwa upande wake, Meneja wa CRDB Kanda ya Kusini, Denis Mwoleka, amesema benki hiyo imeanzisha kampeni ya miaka mitatu ijulikanayo kama “Keti Jifunze”, yenye lengo la kusaidia shule mbalimbali nchini kwa kutoa meza na viti, ili kuunga mkono jitihada za Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuendeleza sekta ya elimu.

Mwoleka ameongeza kuwa kampeni hiyo itazifikia shule zote katika kila Halmashauri nchini, ili kuhakikisha kila mwanafunzi anapata mazingira bora ya kujifunzia na kuimarisha ubora wa elimu.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • DED MADABA APIGA KURA KATIKA KITUO CHA SHULE YA MSINGI KIFAGURO

    October 29, 2025
  • MAFUNZO YA WASIMAMIZI WA VITUO NA WASIMAMIZI WASAIDI YAFUNGWA RASMI, MSISITIZO WAWEKWA KWENYE UZALENDO NA UADILIFU.

    October 27, 2025
  • WASIMAMIZI WAKUU WA VITUO VYA UCHAGUZI NA WASIMAMIZI WASAIDIZI WAPIGWA MSASA MADABA

    October 26, 2025
  • MKUTANO MKUU WA 32 WA WINO SACCOS WAFANA MADABA

    October 25, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa