• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

HALMASHAURI ya Madaba waagizwa kujenga viwanda vya kuongeza thamani mazao

Posted on: November 26th, 2022

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Madaba kutenga maeneo ya kujenga viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya miti.

Kanali Thomas ametoa ushauri huo wakati anazungumza watendaji wa Halmashauri hiyo kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Madaba.

Amesema hali ya hewa ya Madaba inafaa kwa mazao ya miti,parachichi na tangawizi hivyo vikianzishwa viwanda kuongeza thamani ya mazao hayo wananchi watapata faida maradufu. “Anzisheni pia mashamba ya pamoja (block farming) ,wakulima watapata fursa ya kulima zao la aina moja hivyo kuongeza uzalishaji na kuinua uchumi “, alisema.

Mkuu wa Mkoa pia amewaagiza watendaji kuhakikisha mbolea ya ruzuku inawafikia wakulima jirani na maeneo wanayoishi.

katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa amewaagiza watendaji katika Halmashauri ya Madaba kusimamia utekelezaji wa miradi ili iweze kukamilika ndani ya mkataba.

Amesema Rais Samia Suluhu Hassan anatoa mabilioni ya fedha kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo hivyo ni lazima miradi itekelezwa kwa viwango ndani ya mkataba .

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Madaba Sajidu Idrisa Mohamed amepongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa zaidi ya shilingi bilioni 2.1 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya Halmashauri hiyo. 

Amesema hospitali ya Madaba inatarajia kuanza kutoa huduma za afya wakati wowote ambapo serikali tayari imefunga mashine ya X-ray yenye thamani ya shilingi milioni 350. 

Ameongeza kuwa katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 serikali imetoa shilingi bilioni 186 kwa ajili ya kulipa malimbikizo ya watumishi 127 katika Halmashauri ya Madaba.

Halmashauri ya Madaba yenye watumishi 616 ina upungufu wa watumishi 407. 

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma 


Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa